• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkutano kati ya Tanzania na Msumbiji

Tarehe ya kuwekwa: August 2nd, 2017

MKUTANO WA UJIRANI MWEMA KATI YA TANZANIA NA MSUMBIJI ULIVYOIMARISHA USHIRIKIANO
MKUTANO wa ujirani mwema kati ya Tanzania na Msumbiji uliofanyika kwa siku mbili kuanzia Julai 23 hadi 24 mwaka huu kwenye hoteli ya Hunt Club Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma nchini Tanzania, umeimarisha mahusiano, undugu na kujenga ushirikiano baina ya nchi husika.

Katika mkutano huo maazimio 12 yanayozihusu nchi hizo yamepitishwa na yanahitaji utekelezaji ambao utaonesha matokeo makubwa katika maeneo ya Utawala bora, uchumi,biashara,ulinzi na usalama.

Maazimio ambayo yamepitishwa katika kikao hicho ni kuwaelimisha wananchi wanaovuka mipaka kutumia mipaka halali ili wananchi watumie mipaka na kuwezesha serikali zote kupata kodi,kuajiri wafanyakazi wenye weledi na masuala ya forodha na wafanyabiashara toka pande zote mbili kuanzisha maonyesho ya biashara ya ndani na nje ya nchi husika.

Maazimio mengine yaliopitishwa ni kutambua vituo vya mipakani viwe rasmi,kuwe na kituo cha pamoja ili kuboresha mazingira bora ya biashara,kuimarisha  na kulinda mazingira kupitia mradi wa bonde la ziwa Nyasa na kutambua mapito muhimu ya wanyamapori ili kuzuia ujangili.

Kikao hicho pia kimepitisha maazimio ya kuzuia wizi wa pikipiki kupitia mipakani baina ya nchi hizo,wizi wa uuzaji wa silaha toka nchi zote,ununuzi wa boti katika mpaka wa Kilambonamoto ambao ulikuwa unafanyakazi upande wa Tanzania  ili boti hiyo ianze kazi upande wa Msumbiji.

Maazimio mengine yaliopitishwa katika kikao hicho ni vikosi kazi vya usalama katika nchi husika kushirikiana kuchunguza wageni wanaoingia katika nchi hizo ili kuzuia viashiria vya uwepo wa matukio ya ugaidi.

Pia mkutano huo wa siku siku mbili  umepitisha  uwepo wa uvunaji  haramu wa maliasili za madini ili ufanyike ufuatiliaji wa mara kwa mara kuwafuatilia wahusika wakamatwe na kuhukumiwa kulingana na sheria za nchi husika.

Mkutano huo umehudhuriwa na wakuu wa wilaya na mikoa ya Ruvuma na Mtwara kwa upande wa Tanzania na wakuu wa wilaya na magavana wa majimbo ya Niassa na CaboDelgado kwa upande wa Msumbiji.

Kikao hicho muhimu pia kimehudhuriwa na mabalozi wa Tanzania nchini Msumbiji na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania.

Hiki ni kikao cha tatu cha ujirani mwema kufanyika baina ya nchi husika. Mkutano wa kwanza ulifanyika mkoani Mtwara nchini Tanzania, Mkutano wa pili ulifanyika Pemba jimbo la CaboDelgado nchi Msumbiji ambapo mkutano wa nne unatarajiwa kufanywa Novemba mwaka huu katika Jimbo la Niassa nchini Msumbiji.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa