• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA RUVUMA AKABIDHI HATI MILIKI YA ENEO LA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA UHASIBU ARUSHA - TAWI LA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: June 16th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

16 JUNI 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi Wilbert Ibuge amekabidhi hati miliki ya eneo la jumla ya hekari 65 lililopo Kata ya Tanga Mtaa wa Pambazuko Manispaa ya Songea kwa ajili ya ujenzi wa chuo kikuu cha Uhasibu Arusha-Tawi la Songea hapo jana Juni 15, 2022.

Akizungumza wakati akimkabidhi hati miliki hiyo, Brig. Jen Ibuge “ameishukuru Serikali ya Awamu ya 6 kwa kuhakikisha inatoa fursa ya kuwezesha wananchi kunufaika katika nyanja tofauti ambapo kupitia Wizara ya Elimu zitatolewa fedha ambazo zitasaidia kukamilisha ujenzi wa chuo hicho Mkoani Ruvuma ambacho kitakuwa na uwezo wa kuwa na wanafunzi zaidi ya elfu nne (4000)”.

Ametoa wito kwa Mkuu wa chuo hicho kuhakikisha wanaanza hatua za awali za ujenzi kwa kuwa baadhi ya changamoto zilizokuwa zinakabili eneo hilo ikiwemo na ukosefu wa umeme na maji tayari zimeshatatuliwa na mamlaka husika.

Ibuge ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuendelea kushikamana kwa kuhakikisha wanashiriki katika maendeleo chanya ya Mkoa wa Ruvuma ambapo kupitia ujenzi wa chuo hicho utafungua fursa ya ajira pamoja na kuongeza kipato kwa biashara.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Mwaitete Cairo ametoa shukurani kwa uongozi wa Mkoa wa Ruvuma ambapo alisema kuwa ujenzi wa chuo hicho utasaidia kupunguza uhitaji wa elimu ya juu kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kwa kuunga mkono jitihada za Serikali pamoja na sera ya nchi inayozingatia utoaji wa elimu bora kwa wananchi.

Aliongeza kuwa ujenzi wa chuo hizho unatarajia kuanza rasmi mwezi Julai 2022 ambapo hadi sasa hatua za awali za ujenzi zimeanza ikiwemo na uandaaji wa michoro ya ujenzi huo.

Naye Makamu Mwenyekiti wa bodi ya chuo cha Uhasibu Arusha CPA Joseph Mwiguru alisema kuwa chuo kimejipanga kutoa elimu bora kwa wanafunzi watakaodahiliwa katika chuo hicho wa ndani ya Mkoa pamoja na nchi jirani na Mkoa wa Ruvuma.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songea Hamisi Abdallah Ally ameahidi kutoa ushirikiano kwa uongozi wa chuo hicho ili kufanikisha ujenzi wa chuo kwa haraka ikiwa ni utekelezaji wa sera ya elimu kupitia Ilani ya CCM ambayo inatoa kipaumbele kwa utoaji elimu kwa wananchi wake.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt Frederick Sagamiko alisema Manispaa ya Songea imekamilisha hatua ya upimaji wa eneo pamoja na uandaaji wa hati miliki.

Mwisho.

  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa