• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amewataka Waandishi wa Habari kutumia taalma zao vizuri katika kuandika Habari.

Tarehe ya kuwekwa: November 20th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewataka waandishi wa habari kutumia taaluma zao kwa ustadi na kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa waandishi wa habari na wadau mbalimbali yaliyofanyika katika ukumbi wa HOMSO tarehe 19 Novemba 2024  na kuendeshwa na Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kanali Ahmed aliwasihi waandishi kutii misingi ya maadili ili kutoa habari zilizo sahihii.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa alitoa rai kwa viongozi wa chama hicho kuendelea kuwahimiza waandishi wanaokwenda kinyume na maadili ya tasnia ya uandishi wa habari, ili waonyeshwe njia sahihi ya kuandika na kutekeleza jukumu lao.

Alisema kuwa ni muhimu kwa waandishi kuendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kujitokeza kwa wingi katika upigaji kura, hususan katika uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa, utakaofanyika tarehe 27 Novemba 2024.

Wakili Dickson Ndunguru, ambaye ni wakili wa kujitegemea, alizungumzia umuhimu wa uhuru wa kujieleza na kusema kwamba ni haki ya kila mtu au jamii kueleza mawazo na maoni yao.

Alisisitiza kuwa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa uhuru wa kujieleza, huku akieleza kuwa sheria nyingine kama vile sheria ya magazeti, usalama, na msaada wa habari zinahitaji kuzingatiwa ili kuhakikisha uhuru huu unatumika ipasavyo.

Aliongeza kuwa uhuru wa kujieleza ni muhimu kwa jamii katika kukuza uwajibikaji na maendeleo.

Kwa upande mwingine, Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Shekhe Ramadhani Mwakilima, alitoa maoni yake kuhusu uhuru wa kujieleza kutoka katika mtazamo wa kidini ambapo alisisitiza kuwa dini haitoi kikwazo kwa mtu kujieleza, lakini inasisitiza kwamba kila mtu anapaswa kutumia uhuru wake kwa njia inayojenga umoja na si kutenganisha jamii.

Mafunzo haya, yaliyojumuisha waandishi wa habari na wadau mbalimbali, yalilenga kukuza na kuimarisha uhuru wa kujieleza, huku wakihimiza umuhimu wa maadili na sheria katika tasnia ya habari.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa