• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA RUVUMA KUHIMIZA UKUSANYAJI WA KODI ZA MAJENGO.

Tarehe ya kuwekwa: March 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewataka Wataalamu kufanya kazi kwa weredi na kutekeleza vizuri jukumu la kukusanya kazi data za walipa kodi za majengo, mabango na kugawa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo.

Christina ametoa agizo hilo  jana 12 machi 2021 kwenye kikao kilichohudhuriwa na Wakurugenzi wa Halmashauri zote Mkoani Ruvuma, Maafisa biashara, Maafisa Tehama, pamoja na makatibu tawala kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo katika kufanikisha kwa zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo kwa kutumia mfumo wa ulioandaliwa na ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na mamlaka ya Mapato Tanzania TRA.

Alisema awali kodi za majengo zilikuwa zikikusanywa na Serikali za mitaa, kuanzia julai mosi 2017 jukumu hilo  walipewa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA kwa sheria ya fedha namaba 4 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2017. kupitia kikao kazi cha tarehe 05 februari 2021 ofisi ya Rais TAMISEMI ilirejesha ukusanyaji wa kodi za majengo, ugawaji wa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo na ushuru wa mabango kutoka kwa mamlaka ya mapato Tanzania kwenda kwa Serikali za mitaa.

Alibainisha kuwa mwaka 2020 Mkoa wa Ruvuma ulipokea vitambulisho 58,000 na kufanikisha kugawa vitambulisho 23256 kwa kutumia mfumo wa ugawaji wa vitambulisho ulioandaliwa na ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo kati ya hivyo vitambulisho   34744 vimebaki.

Akitoa pongezi kwa Halmashauri ya Mbinga ambayo imefanikiwa kugawa vitambulisho 4768 kati ya vitambulisho 6500 sawa na asilimia 53% huku Halmshauri nyingine zikiwa chini ya wastani 50%. Ameagiza Halmashauri zote Mkoani Ruvuma kurudisha haraka vitambaulisho vilivyobakia vya kipindi cha mwaka 2020 ili viweze kurudishwa Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Alisema mwaka 2021 Mkoa wa Ruvuma umepewa vitambulisho 56,000 ambapo tayari mgawanyo wa vitambulisho hivyo umeshafanyika ambapo Manispaa ya Songea imepewa vitambulisho 10600, Tunduru vitambulisho 10200, Namtumbo vitambulisho 7700, Mbinga mji vitambulisho 6300, Mbinga 6300, Nyasa vitambulisho 7700, Madaba vitambulisho 3900 na halmashauri ya Wilaya ya Songea vitambulisho 3300.

Amewataka Wataalamu hao kusimamia vizuri ukusanyaji wa kodi za majengo ikiwemo na utunzaji wa takwimu za mabango sambamba na utoaji wa elimu kwa walipa kodi ili kuwajengea uelewa wananchi wa  ulipaji wa kodi zamajengo, na  mabango.

Mwisho alitoa wito kwa wajasiliamali yeyote atakayekuwa amepewa kitambulisho kutobugudhiwa au kunyanyaswa na mtu yeyote kwani atakuwa ametambulika rasmi kupitia kitambulisho alichokuwa nacho. Alisisitiza.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

13.03.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa