• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA SONGEA, "Akemea uvutaji wa madawa ya kulevya ambao husababisha ngono uzembe."

Tarehe ya kuwekwa: December 1st, 2020

Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Dr. John Pombe Magufuli imejidhatiti katika kuboresha huduma za afya nchini,  ikiwemo  na kutoa huduma za upimaji wa VVU, huduma ya Tohara kwa wanaume, pamoja na kuimarisha kamati za UKIMWI za kata na mitaa ili kutokomeza au kupunguza maambukizi mapya ya Virus vya Ukimwi.

Hayo yametamkwa na  Mkuu wa Wilaya ya Songea  Pololet  kamando Mgema kwaniaba ya Dr. Damas Ndumbaro (Mbunge Jimbo la Songea Mjini)  katika maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 01 disemba Duniani kote, ambayo kiwilaya maadhimisho hayo yamefanyika katika kata ya Mshangano Manispaa ya Songea.

 Awali mgeni rasmi alianza kukagua vibanda vya maonesho mbalimbali vya wadau wa mapambano dhidi ya Ukimwi   ikiwemo na dawati la jinsia na watoto (Ruvuma), Inter Care Organization (ICO), ICHF under five 5, PAD pamoja na banda la upimaji wa virus vya ukimwi (VVU).

Pololet aliwapongeza wale wote waliothubutu kwenda kupima VVU na kujua hali ya afya zao ambapo katika maadhimisho hayo watu 128 walijitokeza kupima VVU,  wanaume 79 na wanawake 49 kati ya hao hakuna aliyekutwa na maambukizi ya VVU.

 Alisema lengo kuu la Serikali ni  kutoa elimu dhidi ya maambukizi ya VVU na namna ya kujikinga na kuwakinga wengine ili maambukizi yasiweze kuenea Zaidi, pamoja na kutoa elimu ya namna ya kuzuia kuenea kwa VVU katika jamii.

Amewaasa wale wote wenye  maabukizo ya Virus Vya Ukimwi  kufuata maelekezo yote yanayotolewa na wataalamu wa afya ikiwemo kuanza dawa mara moja na kwa usahihi bila kuacha.

Akizitaja faida za kupima na kutambua afya zao ambapo alisema,  itawasaidia kujiunga na  kupata dawa za kufubaza makali ya  VVU (ARV), atakuwa amepata maelekezo ya matumizi sahihi ya dawa za ARV hususani  ( wamama wajawazito), pamoja na kufahamu namna  ya kuzuia maambukizi kwenda kwa wengine. ( Pololet alibainisha).

Naye  Mratibu wa kudhibiti UKIMWI (TIBA) Manispaa ya Songea  Felista Kibena alisema “ katika kipindi cha mwaka 2019 hadi 2020 jumla ya watu  57232 walipimwa afya zao, hivyo  wanaume 33037 na wanawake 24195 kati ya hao wanaume 905 na wanawake 1344 walikutwa na maambukizo ya VVU sawa na asilimia 3.9% na hao wote wamefanikiwa kuunganishwa kwenye huduma ya tiba na matunzo katika vituo vya CTC.”

Kibena aliongeza kuwa katika kipindi cha 2019 hadi 2020 jumla ya akina mama 8572 wamepimwa afya zao na kati ya hao kina mama 166  waligundulika na VVU sawa na asilimia    1.9 %, na wote wameanza dawa za kufubaza makali ya VVU ( ARV).

Aidha, Manispaa ya Songea  inaendelea kutoa Elimu kwa jamii juu ya kujikinga na maambukizo ya virus vya ukimwi pamoja na  kutoa elimu sahihi ya matumizi ya sahihi ya kondomu na kuzisambaza kwa watumiaji kwa kutumia watoa huduma na waelimishaji rika kwa kata zote 21 na mitaa 95.

Kauli mbiu” MSHIKAMANO WA KIMATAIFA, TUWAJIBIKE KWA PAMOJA.”

IMETAYARISHWA NA;                                                                                                                       

AMINA PILLY;

AFISA HABRI MANISPAA YA SONGEA.

01.12.2020 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa