• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA SONGEA AMEWATAKA WANANCHI KUTUNZA VYANZO VYA MAJI

Tarehe ya kuwekwa: April 6th, 2022

Na;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI 

MANISPAA YA SONGEA.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema, amewataka Wananchi wa Manispaa ya Songea kufuata sheria ya Mazingira namba 20 ya mwaka  2004 ambayo inasisitiza kuwa  kutoka  kwenye kingo za Mito  kwa  pande zote mbili hadi mita 60 ni   vyanzo  vya maji.

Kauli hiyo imeelezwa leo tarehe 06.04.2022 wakati akizungumza na Wananchi wa Manispaa ya Songea akiwa katika hatua ya  utekelezaji wa zoezi la upandaji wa miti katika Bonde la Mto Ruhila lililopo kata ya Seedfarm  kwa lengo la kutunza chanzo cha Maji Ruhila ( SOWASA) lililoshirikisha wanafunzi, Waheshimiwa Madiwani, Wataalamu na wananchi.

Pololet alisema “ awali maeneo hayo yalikuwa ni sehemu ya shughuli za kibinadamu pamoja na makazi ya watu,  baadae Serikali ilitoa shilingi Bilioni 1.9 kulipa fidia kwa wananchi wa eneo  la Mabonde kama Mahilo, Chemchem, pamoja na Ruhila  ili kutunza uoto wa asili wa mazingira ya chanzo cha Maji Ruhila.”

Aliongeza kuwa baada ya kuwaondoa wananchi hao, amezitaka  Mamlaka husika kama SOWASA, TFS, pamoja na Idara ya Maliasili kutekeleza wajibu wao  kwa kuweka ulinzi imara wa maeneo  kwa kuweka mipaka inayoonekana,  pia alama hizo zitumike kama katazo la mtu yeyote  kuzivuka na kwenda  kufanya  shughuli za kibinadamu ndani ya eneo linalohifadhiwa.  

Amewarai wananchi wa Manispaa ya Songea hususani waishio jirani na Bonde la la Mto Ruhila  ikiwemo na shule ya Wavulana ya Songea ambayo ipo jirani na bonde hilo kuhakikisha wanaimarisha ulinzi  katika kunza chanzo hicho kwa manufaa ya jamii yote ya Songea.

Amempongeza Waziri wa Sheria na Katiba ambaye pia ni Mh. Mbunge wa jimbo la Songea Mjini pamoja na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Mary Massanja kwa kuwatia moyo wananfunzi wa shule ya Sekondari  ya Wavulana Songea kwa kuanzisha vikundi vya utunzaji wa vitalu vya miti ambapo vikundi hivyo vimeweza kuatika miche ya miti   elfu hamsini 50,000 ambayo imetumika kupandwa katika bonde la mto Ruhila. Pololet “ alipongeza”

Amemtaka  Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea kushirikiana  na  Taasis mbalimbali kama TFS, na Idara ya Maliasili ambayo ipo chini ya Halmashauri,  kuhakikisha wanaotesha miche ya miti na kuweka Mpango thabiti kwa kila mkuu wa Idara aweze kupewa kata kwa kushirikisha   waheshimiwa Madiwani wa kata husika  kuhakikisha upandaji wa miti unafanyika samabamba na kutunza miti hiyo. Alisisitiza.

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano, amewataka wananchi wote wa Manispaa ya Songea kuhakikisha wanapanda miti aina ya miparachichi ambayo itasaidia kuinua kipato cha familia.

Afisa Misitu Manispaa ya Songea Godfrey Luhimbo, amesema miti iliyopandwa katika chanzo cha Maji Ruhila itasaidia kuweka mazingira mazuri ambayo yataweza kuimarisha uoto wa asili, ikiwa katika zoezi hilo   miti aina ya Minyonyo 3000  imepandwa.

Nao wanafunzi wa Shule ya Wavulana Songea kwa umoja wao wamesema wataitunza miti hiyo kwa kuhakikisha  isiweze kuungua  moto kwa manufaa ya jamii ijayo.

Mwisho.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa