• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA SONGEA AMEWATAKA WATAALAMU KUANDAA DCC KWA AJILI YA WASILISHO LA MADINI, MISITU NA ARDHI.

Tarehe ya kuwekwa: January 20th, 2024

Wilaya ya Songea ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe. Kapenjama Ndile  wamefanya kikao cha kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Songea ambacho kimefanyika tarehe 19 Januari 2024 kwa lengo la kufanya tathimini ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali Wilayani humo pamoja na kupokea ushauri na changamoto zilizojitokeza ngazi ya Wilaya ya Songea.

Kikao hicho kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya, Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Songea, Wenyeviti wa Halmashauri ya Madaba, Songea, Manispaa ya Songea, Wakuu wa Idara, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini pamoja na wadau mbalimbali kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe. Wilman Kapenjama Ndile amesema, Serikali imetengeneza  utaratibu na miundo mbalimbali  wa kukutana na  kukusanya mawazo na ushauri kutoka kwa wadau hususani kwa  Wilaya husika ambapo huwezesha kutatua changamoto na kuleta maendeleo kwa jamii.

Alisema Serikali imejipanga kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Wilaya ya Songea kwa kuhakikisha wanapeleka huduma muhimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali hasa miundombinu ya umeme, maji, elimu na afya, mazingira  na kilimo hususani zao la Miwa. “Alibainisha.”

Aliongeza kuwa kupitia kiwanda cha miwa kinachotarajia kujengwa katika kijiji cha Magwamila katika  Halmashauri ya Wilaya ya Songea kitawezesha  kuniua pato la Taifa, Kuimarika kwa  miundombinu ya barabara pamoja na fursa za ajira kwa Wananchi.

Aidha amewataka wataalamu kuandaa kikao kingine ambacho kitalenga kuandaa wasilisho la Sekta ya madini ngazi ya Wilaya  ambayo itasaidia kufahamu kupata takwimu ya misitu iliyopo, ikiwemo na sekta ya ardhi katika zoezi la  upimaji wa ardhi ambao utawezesha  kufahamu idadi ya viwanja kulingana na  ongezeko la jamii inayohitaji  viwanja.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Songea Mjini Mwinyi Msolomi amewataka wataalamu kuandaa mpango kazi wa utekelezaji wa maendeleo  wa mwaka mmoja ambao utawasilishwa katika kikao na kujadiliwa ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali za jamii kupitia Halmashauri husika.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakurugenzi wa Halmashauri zote 3 zilizopo ndani ya Wilaya ya Songea, ambapo  wameahidi kusimamia kikamilifu utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri zao.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa