• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA SONGEA ATOA ELIMU YA SENSA KWA KAMATI NGAZI YA WILAYA.

Tarehe ya kuwekwa: June 13th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

13 JUNI 2022

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ameongoza kikao kazi cha kamati ya Sensa ya Wilaya ya Songea leo tarehe 13 Juni 2022 kwa lengo la kupokea taarifa ya maandalizi ya sensa ya watu na makazi katika Wilaya ya Songea.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini, viongozi wa mila pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Akizungumza katika kikao hicho, Mgema ameitaka kamati hiyo inaleta ushirikiano katika kuhakikisha wanasimamia zoezi la uhamasishaji  kwa wananchi kwa kutoa elimu kupitia mikutano mbalimbali, nyumba za ibada, mikusanyiko mbalimbali, na vyombo vya Habari kuhusiana na zoezi la SENSA  ya watu na makazi ambalo linatarajiwa kufanyika ifikapo Agosti 23 mwaka huu.

Mgema alisema kuwa kila mwananchi anatakiwa kutambua na kushiriki kikamilifu kwa kutoa taarifa sahihi ikiwemo na idadi ya watu katika kaya husika kwa mujibu wa sheria ya Takwimu kwa lengo la kufanikisha na kuchochea kasi ya maendeleo ya watu na makazi yao. “Mgema Alisisitiza”



Akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya sensa ya watu na makazi Manispaa ya Songea, Mratibu wa sensa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Upendo Bonomali alisema kuwa Manispaaya Songea imetenga maeneo 477 ya kuhesabia watu pamoja na kuunda kamati za sensa ngazi ya kata zote 21 na mitaa 95.

Aliongeza kuwa Manispaa ya Songea imefanya uhamasishaji wa zoezi hilo kwa jamii kupitia matamasha mbalimbali, kugawa vipeperushi vinavyotoa elimu ya sensa kwa jamii, kutoa elimu kwa Madiwani, watendaji wa kata, wenyeviti wa mitaa na mabalozi kupitia vikao mbalimbali pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kupitia vikao vya kisheria katika maeneo yao.

Kwa upande wake Mratibu wa Sensa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Prosper Romanus Luambano alisema kuwa hadi sasa wameandaa maeneo 170 ya kuhesabia, kuhamasisha jamii kupitia vikao mbalimbali vya kisheria, kugawa vipeperushi  pamoja na kuunda kamati za sensa kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji na kata.

Pia, Mratibu wa Sensa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Zainabu Mbaruku Hamidu alibainisha kuwa zoezi la uhamasishaji jamii linaendelea kufanyika kupitia matamasha ya michezo, vikao mbalimbali, mikutano , ugawaji wa vipeperushi pamoja na uundaji wa kamati za sensa kwa ngazi zote.


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano alisema kuwa kamati za kata zinatakiwa kuweka wawakilishi ambao ni viongozi wa dini ili kurahisisha utekelezaji wa zoezi la uhamasishaji kwa jamii.

Naye Katibu wa Baraza la Waislamu Mkoa wa Ruvuma (BAKWATA) Shekhe Rajabu Songambele ametoa shukrani kwa uongozi ngazi ya Wilaya kwa kuandaa kikao cha uandaaji wa kamati ya uhamasishaji wa SENSA ya watu na makazi pia ameahidi kutoa ushirikiano katika kutekeleza na zoezi hilo.

Mwisho.




Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa