• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Songea azindua mkakati wa kutokomeza mbu wa malaria

Tarehe ya kuwekwa: September 21st, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma Pololet Mgema amezindua mkakati wa kutokomeza mazalia ya mbu katika Manispaa ya Songea.

Akizungumza na wananchi katika kituo cha afya cha Mjimwema Mgema amesema Mbu waenezao magonjwa huchangia  kwa kiasi kikubwa kuleta umasikini katika Taifa letu kwani wengi wanaoathirika ni nguvu kazi na tegemeo  katika kujenga uchumi wa Nchi Taifa.

Mgema amezitaja changamoto ambazo wanakumbana nazo ni ushiriki hafifu wa Jamii katika kushiriki kwenye  usafi wa mazingira ili kuondoa uchafu ambao ni vyanzo vya mazalia ya Mbu na tabia ya jamii kutokuchukua hatua za haraka ili kupata matibabu kwenye vituo vya afya pale ambapo wamejiona wamepata maambukizi.

Kwa upande wake Afisa wa Manispaa ya Songea Vitalis Mkomela amesema kutokutumia matumizi sahihi ya chandarua na kutokuzingatia kupima vimelea kabla ya matibabu ni miongoni mwa sababu za kuendelea kwa ugonjwa wa malaria.

Mkomela ameitaja mikakati ya kutokomeza mbu hao  ni kuboresha usafi wa mazingira na kujenga nyumba bora, kuwahi matibabu mapema na ,kufuata ushauri ambao unapewa na Mganga kuhusu magonjwa yaenezwayo na Mbu na kuzingatia matumizi sahihi ya vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu.

“Sio kila homa ni Denguee sio kila homa ni Malaria pima hakikisheni mnapima kabla y kutumia dawa”. Amesisitiza Mkomela.

Naye, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Mameritha Basike amesema wameanzisha zoezi la unyunyuziaji dawa kwa sababu mazalia ya Mbu yameongezeka na kusababisha  ugojwa wa Malaria na dengue na kwamba zoezi la kupulizia mazalia ya mbu litasaidia kutokomeza mazalia yote ya Mbu.

Vile vile amesisitiza kuwa watatoa elimu kwa Jamii kuhusu watu ambao watapita mitaani kufanya kazi ya kuuwa mazaria ya mbu.

Afisa afya wa Manispaa ya Songea Maxensius Mahungi amesema ugonjwa wa dengue umeleta madhara ya vifo katika wakazi wa mikoa 11 ugonjwa wa dengue ulianza Januari 2019 ambapo hadi  Julai 15 kumekuwa na idadi ya  wagonjwa 6518 na vifo sita.

Kulingana ya takwimu Wagojwa wengi wametokea Dar Es Salam 6104, Tanga 312, Pwani,57, Morogoro 22, Lindi 8, Arusha 5, Dodoma3, Ruvuma wawili katka wilaya ya Tunduru, Kagera wawili, Singida wawili na Kilimajaro mmoja.

  Mahundi amesema ugojwa wa dengue unaenezwa na mbu jike aina ya aides mbu mweusi mwenye madoadoa marefu meupe ya kang’aa ambaye huuma wakati wa asubuhi,jioni na kwenye maneo yenye kivuli pia mbu denge hutaga mayai yake katika mazalio ambayo yapo kwenye kivuli cha miti ambayo ni makopo,matairi ya magari yenye maji.

Amezitaja dalili za ugojwa wa dengue kuwa ni kupata homa ya ghafra, kuumwa na kichwa hususani sehem za macho, maumivu ya viungo, kutokwa na damu sehem ya fizi, mdomoni puani na njia ya haja kubwa na ndogo, kichechefu, au kutapika, kuvumba tezi.

Imeandaliwa na

Farida Mussa 

 Wa kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Septemba 18,2019

   

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa