• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA SONGEA MJINI ATOA MAFUNZO KWA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA.

Tarehe ya kuwekwa: October 24th, 2020

Mpiga kura ambaye picha yake haipo/ haionekani katika daftari la wapiga kura lakini ana kadi ya mpiga kura yenye taarifa sawa na zilizopo katika daftari la kudumu la wapiga kura, “aruhusiwe kupiga kura kura”.

Hayo yamebainishwa na Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea Mjini Tina Sekambo akiwa katika ufunguzi wa mafunzo kwa makarani waongozaji wapiga kura yaliyofanyika leo 24 oktoba katika kumbi tofauti mjini  Songea.

Tina amewataka Makarani waongozaji  kufanya kazi kwa weredi na kwa kufuata maelekezo yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kuacha kutumia simu wawapo kituoni ili kutoa huduma bora  kwa wapiga kura sambamba na kutoa maelekezo inapobidi kufanya hivyo na  kwa kutumia lugha   nzuri pamoja na kuweka kipaumbele kwa makundi maalumu kama wazee, walemavu, wajawazito,  wanaonyonyesha na  wagonjwa.

Alisema makarani waongozaji wapiga kura ni watendaji wanaoteuliwa na msimamizi wa uchaguzi kwa ajili ya kuwaelekeza wapiga kura wasioweza kutambua vituo walivyopangiwa.

Aliongeza kuwa Jimbo la Songea Mjini lina vituo vya kupigia kura  393 ambapo kila karani atawajibika kuwepo  kwenye kituo chake mapema kabla ya kufungua kituo ili aweze kujiandaa kutoa huduma kwa wapiga kura.

Alibainisha kuwa ili kuifahamu ipasavyo orodha ya wapiga kura, msimamizi wa uchaguzi atampatia karani mwongozo wa wapiga kura maelekezo ya namna ambavyo orodha hiyo imepangwa. Orodha hiyo itakuwa na idadi ya wapiga kura isiyozidi 450.

Aidha, moingoni mwa majukumu ya makarani waongozaji wapiga kura yaliyotajwa ni pamoja na kupokea wapiga kura nje ya kituo na kuwaelekeza eneo/ chumba watakachopigia kura, kutoa maelekezo kwa wapiga kura namna ya kujipanga katika mistari miwili kwa kuzingatia ( mstari wa wanawake na wanaume), kutoa kipaumbele kwa wenye mahitaji maalmu, pamoja na  kutoa ushirikiano kwa watendaji wa kituo na mlinzi wa kituo ili kufanikisha kazi za upigaji kura kituoni. Tina Alisisitiza.

Mwisho aliwaasa makaranni hao kusimamia uchaguzi vizuri ili uwe huru na wa haki ukiwa unahusisha kuwapatia wapiga kura fursa ya kupiga kura bila kubugudhiwa wala kusumbuliwa wanapokuwa katika vituo vya kupigia kura.

MTAYARISHAJI;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

24 OKTOBA 2020.

                                                      

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa