• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSIMAMO WA Rais waongeza mauzo ya makaa ya mawe Ngaka

Tarehe ya kuwekwa: June 13th, 2018

MAAMUZI ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk.John Magufuli Kuzuia uagiza wa makaa ya mawe toka nje,badala yake watumiaji wote kutumia makaa ya mawe toka Ngaka Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma, kumesababisha soko la makaa hayo kupanda.

Meneja Uzalishaji wa Mgodi wa Ngaka David Kamenya anasema uzalishaji umeongezeka katika kasi ya ajabu toka tani 6000 hadi tani Zaidi ya 50,000 kwa mwezi hivi sasa.

Kamenya anabainisha makaa ya mawe katika mgodi huo  awali yalikuwa yanapatikana mita tano chini ardhini ambapo hivi sasa baada ya uzalishaji kuongezeka madini hayo yanapatikana kati ya mita 40 hadi 50 ardhini.

Kwa mujibu wa Kamenya,makaa ya mawe yanayochimbwa katika mgodi huo yanatengenezwa kwa ukubwa wa kati ya milimita sifuri hadi 450 na kwamba hivi sasa wamepata wateja kutoka viwanda vyote katika nchi nzima kikiwemo kiwanda cha Dangote cha Mtwara ambacho kinanunua kila mwezi tani 8000 za makaa ya mawe.

“Uzalishaji wa makaa ulianza tangu mwaka 2011,eneo letu la uchimbaji lina kubwa wa kilometa kumi za mraba, utafiti wa makaa ya mawe bado unaendelea’’,anasema Kamenya.

 

Meneja Udhibiti Ubora wa Makaa ya Mawe wa Kampuni  ya TANCOAL Bosco Mabena anasema makaa ya mawe ambayo yanazalishwa kwenye mgodi wa ngaka hayana uchafu wa aina yeyote ukilinganisha na makaa mengine nchini na nje ya nchi.

Mabena anabainisha zaidi kuwa wateja wa TANCOAL wanapendelea vipande wa makaa ya mawe vyenye ukubwa wa kati ya milimita sifuri hadi 75 na kwamba wanasafirisha makaa ya mawe toka mgodini hadi bandari kavu Kitai kwa kutumia magari aina ya tipa kabla ya  kupakiwa katika magari ya mizigo na kusafirishwa mikoa mbalimbali.

“Sasa hivi tuna wateja kutoka karibu viwanda vyote vya Tanzania ikiwemo viwanda vya saruji, nguo, karatasi,jipusamu,tangu serikali ilipozuia kuagiza makaa toka nje ya nchi,sasa mambo yanakwenda vizuri kibiashara,serikali imetuwekea bajeti kubwa katika uzalishaji wa makaa yam awe ya Ngaka’’,anasema Mabena.

Utafiti uliofanywa mwaka 2008 unaonesha kuwa makaa ya mawe ya Ngaka yanaongoza kwa ubora Duniani.Katika eneo hilo zimegundulika tani milioni 400 za makaa ya mawe ambazo zinatarajiwa kuchimbwa kwa miaka zaidi ya 50.

Kwa mujibu wa utafiti madini ya makaa ya mawe Ngaka yamesambaa maeneo yote ya Kijiji cha Ntunduwaro na maeneo jirani ya Kata ya Ruanda.

Ukiachia viwanda vya ndani katika nchi nzima,Tayari madini hayo yamesafirishwa katika nchi za Kenya, Zambia na Malawi.

Mgodi wa Ngaka, unamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali ya Tanzania yenye asilimia 30, na Kampuni ya Intra Energy ya Australia yenye

Katika kutekeleza Dira ya Taifa ya mwaka 2025 Tanzania inatarajia kuzalisha umeme wa makaa ya mawe ambayo yameenea katika mikoa ya kusini  hususan mikoa ya Ruvuma,Mbeya Iringa na Njombe.

Sera Taifa ya madini ya mwaka 1997 inasisitiza juu ya sekta binafsi kuendeleza madini ambapo Serikali katika sera hiyo ina jukumu la kuidhibiti,kuikuza na kuiendeleza sekta hiyo.

Sekta ya madini inachangia takribani asilimia 3.5 ya Pato la Taifa,ambayo inakadiriwa kufikia asilimia 10 ifikapo 2025. 

 

Mwandishi wa Makala haya ni Albano Midelo,mawasiliano yake ni albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa