• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA SONGEA AMEWATAKA WAMACHINGA WOTE KUHAMIA KWENYE MAENEO RASMI YALIYOTENGWA IFIKAPO 31.03.2022

Tarehe ya kuwekwa: March 29th, 2022

Imeandaliwa na;

 AMINA PILLY;

 AFISA HABARI,

 MANISPAA YA SONGEA.

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano amewataka wajasiliamali wadogowadogo wote maarufu kama machinga ambao  wanaendesha biashara zao katika maeneo yasiyorasmi wanatakiwa kuhama  kwenye maeneo hayo na kisha  kuhamia kwenye  maeneo yaliyotengwa rasmi  kwa ajili ya biashara za wamachinga ifikapo tarehe 31 Machi 2022.

Hayo yamebainika katika kikao na Waandishi wa habari kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo tarehe 29 machi 2022  kwa lengo la kueleza au kutangaza mafanikio ya utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za Serikali katika kipindi cha januari hadi Machi 2022.

Mbano alianza kwa kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha Bilioni 8.9 kwa ajili ya utekelezaji wa  miradi ya maendeleo katika   Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambapo fedha hizo zimesaidia katika kujenga daraja BP Stesheni, Barabara ya kiwango cha  lami  kutoka BP Stesheni hadi Sanga one kwa thamani ya shilingi Milioni 500, Barabara ya Seedfarm  kilometa  (1) moja kwa thamani ya shilingi milioni 400,  pamoja na uchongaji wa barabara ya Nonga nonga hadi  kata ya Tanga kwa thamani ya shilingi million 400. 

Akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema “kwa awamu nyingine Manispaa ya Songea imepokea kiasi cha shilingi milioni 200 kwa ajili ya kurekebisha miundombinu ya barabara  ikiwemo na ujenzi mpya wa daraja la Misufini  - matarawe ambapo ujenzi huo  utaanza mara baada ya kumalizika nyakati za masika ya mvua. Mbano “alibainisha.”

Aidha, Katika kutekeleza miradi ya Afya Manispaa ya Songea kupitia mapato yake ya  ndani Manispaa ya Songea,  imetenga kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya  Lilambo ambacho kipo hatua ukamilishaji, piatumepokea fedha Milioni 500 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya  ujenzi wa kituo cha afya Msamala  ambacho kipo hatua ukamilishaji, Ujenzi wa kituo cha kituo cha Afya Subira wenye thamani ya shilingi milioni 500 fedha za TOZO ambao  umefikia  hatua ya ukamilishaji, pamoja na kiasi cha shilingi milioni 500  kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambao upo hatua ya utekelezaji.

Akizungumzia upande wa elimu Manispaa ya Songea ilipokea  shilingi milioni 660 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 29 ikiwa madarasa 26 kwa shule za Sekondari pamoja na madarasa 3 kwa shule za Msingi ikiwa ni Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya  UVIKO 19,.

Ametoa rai kwa vyombo vya habari vyote  kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya wazazi kuchangia chakula shuleni  ili wanafunzi waweze kupata chakula shuleni ikiwa [jukumu hilo halikwepeki litabaki kuwa ni la  mzazi. “Mbano alisisitiza”  

Aliongeza kuwa Serikali inaendelea kutoa fedha za Elimu bila Malipo kwa ajili ya kutatua chanagamoto mbalimbali kwa shule za Msingi na Sekondari lakini haimaanishi  mzazi huyo  asichangie  mchango wa chakula shuleni. 

Mwisho, Amewataka wananchi wote wa Manispaa ya Songea kuhakikisha wanafanya usafi wa mazingira kwenye maeneo yao wanayoishi ili mazingira ya mji yawe safi.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa