• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA SONGEA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO.

Tarehe ya kuwekwa: January 27th, 2021

Mstahiki meya Manispaa ya Songea  Michael L. Mbano ameongoza kamati ya Fedha na uongozi katika  ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo iliyofanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 26 hadi 27 januari 2021 na kufanikiwa kukagua miradi mbalimbali ikiwemo na machinjio ya kisasa Tanga.

Awali  akipokea taarifa za utekelezaji wa mradi wa Stendi mpya ya Tanga alisema  “ Lengo la Serikali la  kuweka mradi  wa kituo cha mabasi Songea ni kuongeza mapato katika Taifa letu hususani Manispaa ya Songea ili Halmashauri iwe inauwezo wa kuwa na vyanzo vya makusanyo ya ndani kwa kutatua changamoto za wananchi kama madawati, uwekezaji kwenye zahanati, na madarasa pia alisema endapo hatuta simamia vizuri vyanzo vya mapato ya ndani hatutafanikiwa kukusanya mapato.”Mbano alisema.

Amewaasa wamiliki wa vyombo vya usafirishaji  abiria wote na madereva wote kufuata taratibu zilizowekwa na Serikali na  kuacha tabia ya inayoendelea kufanyika kwa baadhi ya madereva wa mabasi kukatisha safari zao na kuacha kupitia kituo cha mabasi Tanga, endapo watabainika watachukuliwa hatua za kisheria.

Amewapongeza wananchi wote wa Manispaa ya Songea kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kuchangia nguvu zao katika miradi na hatimaye Serikali kuiwezesha miradi hiyo hadi kufikia hatua ya ukamilishaji  ambapo Serikali imetoa fedha za ukamilishaji/ujenzi  wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa nyumba ya mganga  kata ya Mletele,  ujenzi wa madarasa 2 chandarua Sekondari kwa Tsh 20,000,000, ukamilishaji wa vyumba vitatu vya madarasa  S/m Mitendewawa Tsh 17,000,000,   hosteli 1 Chabruma Sekondari na vyumba vitatu vya  madarasa kwa gharama ya Tsh 138,223,235 fedha za EP4R, madarasa  matatu S/m Ruhuwiko pamoja vyoo matundu tisa kwa Tsh 69,900,000  fedha za EP4R,  na ujenzi wa Madarasa matatu  S/m Bombambili kwa gharama ya Tsh 71,000,000 pamoja na vyoo matundu 12.

Alisema mradi wa ujenzi wa Hosteli ya chabruma Sekondari ambayo imegharimu shilingi 80,000,000 kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa mradi huo ambao umefikia hatua ya kukamilika,  unapaswa kutengewa bajeti ili kuwezesha upatikanaji wa vitanda  kwa ajili ya kutatua changamoto inayoikabili shule hiyo.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

27 Januari 2021.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa