• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano amewataka wananchi kutunza Mazingira.

Tarehe ya kuwekwa: January 25th, 2023

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano amewwataka wananchi, Shule  pamoja na Taasis  mbalimbali kuhakikisha wanapanda miti kwenye maeneo yao kwa lengo la kuboresha na kuyatunza  mazingira na kulinda afya za jamii.

Zoezi la uzinduzi wa upandaji miti Kiwilaya lilizinduliwa Katika kata ya Wino kijiji cha Lilondo katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba  mnamo tarehe 01 Januari 2023 ikiwa ni utekelezaji wa kikao cha Wadau wa Misitu ambacho kilitoa maadhimio ya kufanyika kwa zoezi la upandaji wa miti ifikapo tarehe 01 Januari  kila mwaka.

Akibainisha madhara yatokanayo na ukataji wa miti ovyo ni pamoja na uvutaji wa hewa ukaa, uwepo wa joto kali, jangwa,  upungufu  wa mvua,  Saratani, njaa, pamoja na madhara mbalimbali ya kijamii na kimazingira. “ Mhe Mbano alibainisha”

Aliongeza kuwa miti ni uhai hivyo hatuna budi kupanda miti na kuitunza, pamoja na kuvuna miti kwa kufuata utaratibu uliowekwa ikiwemo na kupata kibali kutoka kwenye mamlaka husikapamoja  na kudhibiti madhara ya moto yasiweze kutokea. “Alisistiza” .

Hayo yamejili wakati wa upandaji wa miti uliofanyika leo tarehe 25 Januari 2023 kaika chanzo cha Mto Ruhila ulioshirikisha wadau wa mazingira TFS, Souwasa, Waheshimiwa Madiwani, Wataalamu, pamoja na Wananchi mbalimbali kutoka kwenye kata husika.

\

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Somgea Beno Philipo Mpwesa amesema lengo ni kuikumbusha jamii juu ya wajibu wa kuhifadhi mazingira kwa kupanda miti pamoja na kutunza vyanzo vya maji kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Beno alisema kuwa Manispaa ya Songea imejiwekea  mikakati mbalimbali ya kupanda  miti  kila mwaka ambapo kwa mwaka 2022 ilipandwa miti 2500,  na mwaka 2023 imepandwa miche ya miti 2500 katika chanzo cha mto Ruhila katika mtaa wa Unangwa kata ya Seedfarm.

Akibainisha mikakati itakayosaidia  kuhifadhi na kuboresha misitu na vyanzo vya maji ni pamoja na kutoa elimu na kuhamasisha wananchi juu ya upandaji wa miti, kuendelea kushirikiana na Taasis na wadau mbalimbali katika kuhifadhi misitu, kuhamasisha na kuwaelimisha  wananchoi juu ya utengenezaji wa majiko sanifu ili kupunguza kasi ya ukataji wa miti, kuanzisha bustani za miche ya miti na matunda , pamoja na kufanya doria maramara ili kudhibiti waharibifu.

Naye Godfrey Luhimbo Afisa Misitu Manispaa ya Songea  alisema lengo la kupanda miti katika chanzo cha maji Ruhila ni  kwa lengo la kuendeleza  chanzo cha Maji SOUWASA ili mazingira yaweze kuimarika  na kuepuka kutokea kwa jangwa ambalo linaweza kuathiri mazingira.

Godfrey alibainisha kuwa mwaka 2022 Manispaa ya Songea ilipanda miti 2500 ambapo kwa mwaka 2023 manispaa ya songea imepanda miti 2500 katika chanzo cha maji SOUWASA na miche ya miti 15,000 imepandwa katika shule, Mitaa 95, na kata 21.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Mtaa Kuchile Ally Shafii amesema wanaishukuru Serikali kwa kuja kupanda miti kwenye chanzo cha maji Ruhila na wameahidi kuyasimamia maeneo hayo kwa  kufanya doria.


IMEANDALIWA NA 

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI. 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa