• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENGE WA UHURU WAMULIKA MIRADI YENYE THAMANI ZAIDI YA BIL 1 MANISPAA YA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: April 13th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

13.04.2022

Kiongozi wa mbio maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Sahili Nyanzabara Geraruma amezindua na kukagua jumla ya miradi 9 yenye thamani ya Shilingi Billion 1,218,600,000 ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea ikiwa ni fedha kutoka Serikali kuu, tozo na mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na nguvu za wananchi.

Akizungumza mara baada ya kufanya ukaguzi wa shughuli za ujenzi unaoendelea wa viwanda vidogo vya wajasiriamali kata ya Lilambo, kiongozi huyo  ametoa wito kwa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kuendelea kujitokeza na kuomba mikopo ili waweze kujikwamua kiuchumi wao binafsi pamoja na Taifa kwa ujumla.

Geramura ameipongeza Halmashauri ya Manispaa Songea kwa kuhakikisha watu wa makundi maalumu wanaendelea kunufaika na asilimia 10% ya fedha kutoka mapato ya ndani kwa kutoa mikopo bila riba pamoja na  kusimamia utekelezaji wa ujenzi wa viwanda ambavyo vitatoa fursa za ajira kwa wanakikundi na wananchi kwa ujumla.

Amewataka viongozi kuendelea kusimamia na kuhakikisha ujenzi wa viwanda hivyo unazingatia ubora unaotakiwa ambapo hadi sasa majengo 5 tayari yamekamilika ikiwemo na kiwanda cha kuchakata mazao ya nyuki,  kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti, kiwanda cha kutengeneza batiki, kiwanda cha ushonaji nguo pamoja na kiwanda cha kuchomelea vyuma na Aluminium.”Alisisitiza”

Aidha, miradi mingine iliyotembelewa na Mbio maalumu za Mwenge wa Uhuru ni pamoja na uzinduzi wa madarasa 2 shule ya Sekondari Lizaboni, kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara katika eneo la bohari ya Serikali, kuweka jiwe la msingi Kituo cha Afya Msamala pamoja na ukaguzi wa mabanda ya rushwa, dawa za kulevya na elimu ya sensa, ambapo miradi yote imeridhiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru.

Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 inasema “SENSA NI MSINGI WA MIPANGO YA MAENDELEO, SHIRIKI KUHESABIWA TUYAFIKIE MAENDELEO YA TAIFA”

Mwenge wa Uhuru Manispaa ya Songea umepokelewa tarehe 12 Aprili 2022 katika kijiji cha Likuyufusi na kukabidhiwa Halmashauri ya Wilaya Madaba 13 Aprili 2022.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa