• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru waweka jiwe la msingi mradi wa maji Mitendewawa

Tarehe ya kuwekwa: June 11th, 2018

MTAA wa Mitendewawa uliopo katika Kata ya Mshangano Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, ni mojawapo katika Mitaa 10 ya awali ambayo imetekeleza Ujenzi wa miundombinu ya maji. Mradi huu wa maji katika Mtaa wa Mitendewawa uliibuliwa na Wananchi wenyewe mwaka wa fedha 2014/2015 na kuanza kujengwa mwaka wa fedha 2016/2017 Mkandarasi akiwa ni Mkongo Building and Civil works Co.Ltd. Mradi huu unatarijiwa kukamilika Juni 30 mwaka huu,

Ujenzi wa mradi huu ulikadiriwa kugharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 517,hata hivyo hadi  sasa Mkandarasi ameshalipwa  zaidi ya shilingi milioni 125 ambazo zimetumika katika Ujenzi wa miundombinu ya maji.Wananchi wanatakiwa kuchangia  asilimia tano ya Mradi sawa na zaidi ya milioni 25 ambayo itatumika kwa ajili ya usimamizi na uendeshaji wa mradi baada ya kukabidhiwa. Kulingana na taarifa ya mradi huo hadi sasa shilingi 124,000 zimeshakusanywa na wananchi.

Kazi zilizopangwa na kukamilika katika Ujenzi wa mradi huu ni pamoja na ;

  • Ujenzi wa Nyumba ya mitambo moja,
  • Ujenzi na ufungaji wa mfumo wa umeme unaotumia mionzi ya jua
  • Ujenzi wa bomba kuu km 0.15
  • Ujenzi wa tanki la kuhifadhi maji lenye ujazo wa lita 45,000
  • Ujenzi wa bomba za kusambazia maji km 13.5
  • Ujenzi wa vituo 13 vya kuchotea maji.
  • Ujenzi wa mfumo wa uvunaji maji ya mvua.

Watu wapatao 3,200 kutoka mitaa ya Mitendewawa na  wanatarajiwa kunufaika na mradi huu kwa kupata huduma ya maji safi na salama.Wananchi wanaishukuru serikali kwa kutekeleza mradi huu wa Maji ambao utasaidia wananchi kupata huduma ya maji safi na salama sehemu ya karibu na makazi yao.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018 Charles Kabeho ameweka jiwe la msingi katika mradi huu ambapo ametoa wito kwa watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi Manispaa ya Songea kuhakikisha eneo ambalo limejengwa tanki la maji ambalo ni mali ya Chama Cha Mapinduzi linapata miliki kamili ili liwe chini ya serikali.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Juni 11,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa