• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENYEKITI ALAT MKOA WA RUVUMA HATUA KWA HATUA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Tarehe ya kuwekwa: December 23rd, 2021

Na; 

AMINA PILLY;

MWANDISHI – ALAT MKOA WA RUVUMA.

23 Desemba  2021.

ALAT ni Jumuiya za Tawala za Mitaa Tanzania ambayo inatekeleza moja ya  majukumu yake kama kujadili masuala mbalimbali yanayohusu Serikali za Mitaa na kubadilishana mawazo, uzoefu, ujuzi baina ya wajumbe.

Katika kutekeleza hilo ALAT Mkoa wa Ruvuma ikiongozwa na Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbinga Mji Mheshimiwa Kelvin Mapunda alifanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali  katika Halmashauri ya Madaba iliyo jumuisha Wenyeviti wa Halmashauri zote 8 zilizopo Mkoani Ruvuma, Wakurugenzi wote, wajumbe mbalimbali wa ALAT Mkoa wa Ruvuma iliyofanyika hapo jana tarehe 22 desemba 2021.

Mh. Kelvin alisema lengo la kufanya ziara  ya kutembelea miradi katika Halmashauri ya Madaba ni kukuza ufanisi na kuhimiza uwajibikaji kwenye mfumo wa Serikali za Mitaa Mkoani Ruvuma ambapo walifanikiwa kutembelea miradi ya vikundi mbalimbali vya ujasiliamali, Miradi ya Maendeleo pamoja na mradi wa uwekezaji wa kampuni Silverlands Tanzania LTD  uliopo Halmashauri ya Madaba.

Aidha, baada ya kutembelea miradi ya vikundi  vya wajasiliamali ALAT Mkoa wa Ruvuma walibaini baadhi ya changamoto ambazo zinakwamisha ufanisi  wa utekelezaji wa vikundi hivyo ambavyo ni pamoja na upungufu wa mitaji ya kutosha kwa ajili ya kuendeshea biashara zao, Baadhi ya vikundi kukosa maeneo ya kufanyia biashara zao, pamoja na ukosefu wa elimu ya ujasiliamali kwa baadhi ya vikundi.

Katika kutatua changamoto hizo Wajumbe hao walishauri Halmashauri ya Madaba kufanya utaratibu wa kuendelea  kuwawezesha wanavikundi hao ili kuinua kipato chao, pia  wataalamu waisaidie jamii katika  kuandaa andiko la mradi husika ambao utakuwa na bajeti halisi ya mahitaji ya kikundi chao.

Miongoni mwa miradi ya maendeleo iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa madarasa matatu 3 na ofisi moja ya Walimu  katika shule ya Sekondari Madaba uliojengwa kwa gharama  ya shilingi milioni 60 fedha za Mpango wa Maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 ambao ulianza tarehe 04 Novemba 2021 kwa kufuata utaratibu na muongozo wa serikalini uliotolewa na kukamilika kwa asilimia 100%.  

Alisema Mamlaka za Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma zitaendelea kusimamia shughuli za maendeleo ya jamii kwa kuzingatia dira ya Taifa ya mwaka 2000 hadi 2025 kwa lengo la kuimarisha mahusiano na uwajibikaji katika Halmashauri hizo na kuimarisha uchumi wa pamoja Mkoani Ruvuma.

Amewataka Viongozi kufanyakazi kwa bidii pamoja na kushirikisha jamii katika vikao vya maamuzi na kuandaa mipango ya utekelezaji wa miradi, kusimamia ukusanyaji wa mapato kwa njia ya mifumo ili kuzuwia mianya ya uvujaji wa mapato na ubadhilifu wa fedha, kuhimiza utendaji kazi shirikishi kati ya wataalamu na madiwani ili katika tafsiri ya uhalisia wa utekelezaji wa miradi ambao ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Naye katibu wa ALAT Mkoa wa Ruvuma Grace Quintine ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbinga Mji  aliwapongeza wataalamu wote wa Halmashauri ya Madaba kwa kusimamia utekelezaji wa ujenzi wa madarasa ya Mapango wa Taifa na mMapambano dhidi ya UVIKO 19 ambao umetekelezwa kwa 100% na kwa wakati uliopngwa na Serikali.

Quintine ametoa rai kwa walimu wa shule mbalimbali ambao wameshiriki kusimamia ujenzi wa madarasa hayo kusimamia miundombinu ya shule ili  isiweze kuharibiwa na wanafunzi.

Mwisho. 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa