• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENYEKITI ALAT RUVUMA AMEZITAKA HALMASHAURI KUSIMAMIA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

Tarehe ya kuwekwa: August 20th, 2024

ALAT ni Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania ambayo iliundwa kikatiba  mwaka 1984 Desemba na kuanza kutumika rasmi mwaka 1985 kwa lengo la kupigania haki za Halmashauri na kuwa sauti moja katika kuleta maendeleo ya Halmashauri  na kufanya mawasiliano ya karibu na Serikali kuu.

Aidha, ni Chombo kinachowezesha  kukuza maendeleo ya Serikali za Mitaa zilizo  huru na kutoa mchango katika kupeleka madaraka kwa wananchi, kuwasaidia madiwani, Mameya na wenyeviti  katika majukumu yao kama wawakilishi waliochaguliwa kidemokrasia  ambacho  kinatoa uongozi, kuhimiza, kukuza ufanisi, uhuru, uwajibikaji,  uwazi na demokrasia kwenye mfumo wa Serikali za Mitaa Tanzania na kwingineko duniani.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Kelvin Mapunda alisema “ anamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha nyingi za miradi kwenye Halmashauri Mkoani humo, ambapo  amewataka viongozi hao, kuhakikisha wanasimamia utekelezaji wa miradi hiyo inayoendelea  kujengwa kwenye Halmashauri mbalimbali  na pia  wahakikishe miradi hiyo inakamilika  kwa wakati.”

Ametoa Rai kwa viongozi wa Halmashauri zote Mkoani Ruvuma kusimama imara katika kukusanya mapato ya Halmashauri kwa lengo la kuleta maendeleo yenye tija  kwenye Halmashauri zao. “ Mhe. Kelvin alisisitiza”

Aliongeza kuwa, Umoja na Mshikamano katika utendaji kazi ni nguzo ya Msingi hivyo amewataka wajumbe hao kuendelea kudumisha ushirikiano   hususani katika kipindi  hiki cha kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Akitoa  pongezi kwa  Wakurugenzi wote Mkoani Ruvuma, kuendelea kushirikiana  katika Jumuiya hiyo ambayo inawawezesha kufanyika  kwa vikao vyote vya kikatiba ndani ya mwaka husika ambapo amesema kufanyika kwa vikao hivyo kunapelekea Halmashauri kupata mafanikio ya kiutendaji ambapo pia  amezitaka  Halmashauri zote Mkoani Ruvuma  kwenda kujifunza  Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika namna ya uendeshaji wa   Biashara ya Kaboni. “Alisisitiza.”

Kikao hicho kimefanyika katika Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma tarehe 19/08/2024 katika ukumbi wa Wilaya ya Tunduru ambacho kilihudhuriwa na Wajumbe wa Jumuiya hiyo kutoka kila Halmashauri Mkoani Ruvuma kwa lengo la kufanya ufutiliaji wa utekelezaji wa shughuli  na kujadili taarifa mbalimbali za maendeleo ambacho hufanyika kila robo moja ya mwaka.

Wakizungumza na chanzo hiki cha habari,  wajumbe hao wamesema”wanamshukuru  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa kutoa kibali cha kufanyika kwa vikao vya kamati hiyo,  ambavyo vinawasaidia  kukutana kwa pamoja na kujadili maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma kupitia Halmashauri zao, ikiwemo na mafanikio ya Ziara ya Katavi ambayo wajumbe hao, walijifunza  namna ya uendeshaji wa Biashara ya Kaboni ambapo wameahidi kuyafanyia kazi kwa vitendo.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY

ALAT RUVUMA.




Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa