• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA KUZALIWA KWA CCM " Panda Miti, Kulinda na Kutunza Mazingira"

Tarehe ya kuwekwa: January 29th, 2023

Miche ya Miti 350 imepandwa katika viwanda vidogo Lilambo, Kituo cha Afya Lilambo, na Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM miaka 46 ambayo huadhimishwa  ifikapo tarehe 05 Februali ya  kila mwaka.

Uzinduzi wa maadhimisho hayo umefanyika tarehe 28 Januari katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea katika kata ya Tanga ambayo imeadhimishwa kwa kutembelea miradi ya Maendeleo na kujionea uhalisia wa hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi.

 Ziara hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti  wa CCM Mkoa wa Ruvuma  Komredi  Oddo Mwisho  ambayo itahitimishwa siku ya kilele katika Wilaya ya Tunduru tarehe 05 Februari ikiwa na lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na uwekezaji wa viwanda vidogo Kata ya Lilambo ambapo vikundi 11 vilikopeshwa zaidi ya Mil. 465 iliyotolewa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na ununuzi wa vitendea kazi, ujenzi wa kituo cha afya kata ya Lilambo uliojengwa kwa gharama ya Mil 500 fedha za mapato ya ndani ambao umeanza kutoa huduma ya awali.

Miradi mingine iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa barabara ya HEROES hadi Mjimwema km 1 kwa gharama ya shilingi Mil. 500  fedha kutoka Serikali kuu ambao ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 ya CCM ibara ya 57 ikiwa na lengo kuu la kuboresha  miundombinu ya usafirishaji na uchukuzi katika kuwezesha shughuli za kiuchumi na kijamii mijini na vijijini.

 Ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa gharama ya shilingi Mil. 500 ambapo mradi upo hatua ya ukamilishaj, ujenzi wa madarasa 6 shule ya Sekondari Lizaboni, ujenzi wa vyumba vya madarasa 4 shule ya Sekondari Lukala pamoja na upandaji wa miti 100 katika Kiwanda kidogo Lilambo, miche ya miti 100 katika Kiituo cha Afya Lilambo na upandaji wa miche 150 katika Hospitali ya Manispaa ya Songea.

Mhe. Mwisho amewataka viongozi ngazi ya Kata na matawi kushirikiana na Maafisa watendaji wa kata na Mitaa katika kutatua suala la wanafunzi wasioripoti shule wa kidato cha kwanza ili kufanikisha Lengo la Serikali la kila mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza lazima aripoti shule.

Ametoa Rai kwa Manispaa ya Songea kuhakikisha viwanda vidogo vilivyopo katikati ya Mji  vihamishiwe kata ya lilambo katika eneo dogo la viwanda, pamoja na kuboresha miundombinu inayozunguka eneo la viwanda hususani Barabara.

Amewapongeza wataalamu wa  Manispaa ya Songea kwa kujenga kituo cha afya Lilambo kilichojengwa kwa fedha za mapato ya ndani ambapo kwasasa kimeanza kutoa huduma za awali pamoja na hatua nzuri za utekelezaji wa miradi ya maendeleo. “MHE. Oddo alipongeza.”

“Amewataka Wataalam wote kuhakikisha wanasimamia na kutunza miti iliyopandwa siku ya uzinduzi wa maadhimisho hayo  ili kutimiza lengo la Ruvuma kuwa ya kijani.” Amesisitiza.

Aidha, katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi  miaka 46, kwa Songea mjini wameweza kusajili wanachama wapya 906. 


IMENDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.






Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa