• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS MENEJIMENT YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA, ATOA AGIZO LA KUHAKIKI MADENI YA WATUMISHI WA MANISPAA YA SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: October 6th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

06.10.2021

Naibu Waziri ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mheshimiwa Deogratius Ndejembi (MB)  amewataka watumishi wa umma kuhakikisha wanafanya kazi kwa ueledi.

Ndejembi ameyasema hayo alipofanya ziara katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea na kuzungumza na watumishi wa umma kutoka Idara mbalimbali ndani ya Manispaa ya Songea leo tarehe 06 Oktoba 2021 kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi hao katika utendaji wao wa kazi.

Akijibu changamoto zilizotolewa na watumishi hao, Ndejembi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya sita imeweka kipaumbele katika kuhakikisha watumishi wote wa umma wanapata maslahi yao ili kuchochea utendaji kazi katika kuleta maendeleo kwa wananchi ambapo miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja upandishaji wa madaraja na mishahara, kutoa ajira kwa walimu hasa walimu wasayansi katika shule za msingi na sekondari, madai ya mishahara pamoja na malipo ya wastaafu kwa kufuata madaraja yao husika.

Ndembeji amewataka watumishi wa umma kuhakikisha wanapodai stahiki na haki zao kwa Serikali na wao wawe wametimiza wajibu wao kama watumishi kwa wananchi wanaowatumikia katika maeneo yao ya kazi kwa kufanya kazi kwa bidii na katika misingi ya nikidhamu na uadilifu.”Alisisitiza”

Ameongeza kuwa ushirikiano kwa watumishi wa umma ni jambo la kuzingatiwa ili kuleta maendeleo yenye tija katika Halmashauri husika lakini pia kwa wananchi wake na kuwataka watumishi  wote kuacha majungu na maneno yasiyofaa mahala pa kazi  na badala yake kuongeza juhudi katika utendaji wa kazi kwa umoja.

Ndembeji amezitaka Halmashauri zote kuhakikisha zinatatua changamoto mbalimbali za wananchi kama vile migogoro ya ardhi pamoja na kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

Pia amemtaka Afisa utumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhakikish anafanya uhakiki wa madeni yote ya Watumishi na hadi  kufikia tarehe 22 Oktoba 2021 awe amewasilisha majina ya watumishi wote wenye madai katika ofisi ya Raisi utumishi.”Alisisitiza”

Ametoa rai kwa watumishi wote wa umma kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO 19 ili kuweza kujikinga na ugonjwa huo ili  kuwa mfano bora kwa jamii inayowazunguka na kuweza kuwahamsisha wananchi  kupata chanjo hiyo.

Kwa upande wake Mheshimiwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano amemshukuru Naibu Waziri huyo kwa kutembelea Halmashauri ya Manispaa ya Songea pamoja na kuhaidi kuyafanyia kazi maagizo yote yaliyotolewa.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa