• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI TAMISEMI AIPONGEZA MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: December 17th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

17.12.2021

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh. David Ernest Silinde amefanya ziara ya siku moja ndani ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 17 Disemba 2021 ambapo katika  ziara hiyo,  aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea, wataalamu pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Manispaa ya Songea.

Silinde alisema  kuwa lengo la kufanya ziara hiyo ni kufanya ukaguzi wa miradi ili kujiridhisha na kuhakiki fedha zilizotolewa na Serikali kiasi cha shilingi milioni 660 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 29 kwa shule za sekondari na vituo shikizi ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea kama zimefanya kazi kama ilivyokusudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Samia Suluhu Hassan.’Alibainisha’

Aliongeza kuwa bilioni 304 zilitolewa kwenye Halmashauri mbalimbali nchi nzima kwa lengo la kujenga miundombinu ya elimu ambazo zimeweza kujenga vyumba vya madarasa elfu kumi na tano (15000) tayari vimejengwa, madarasa ambayo yatasaidia kutatua changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari na vituo shikizi.

Ametoa pongezi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  Dkt. Frederick Sagamiko , wakuu wa shule na kamati za ujenzi kwa usimamizi mzuri   wa miradi ambayo ni  mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 ambao  umekamilika tayari kwa matumizi   kwa asilimia 100%  katika ubora uliotakiwa kama ilivyoagizwa na Serikali.

Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya  Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa miongoni mwa mikakati iliyosaidia  kukamilisha utekelezaji wa miradi ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 kwa asilimia 100% ni pamoja na kufanyika kwa mikutano ya utambulisho wa miradi kwa wananchi,  kukutana na wakuu wa shule na kamati za ujenzi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza mradi kwa wakati, kukutana na wafanyabiashara wauzaji wa  vifaa  vya ujenzi waliopo  Manispaa ya Songea kwa ajili ya kurahisisha ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika utekelezaji wa mradi pamoja na kuunda timu ya ufuatiliaji ngazi ya Halmashauri na kata.’Alibainisha’

Dkt. Sagamiko ametoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Songea kwa kutoa maelekezo thabiti juu ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Kwa upande wake Kaimu Afisa elimu Mkoa wa Ruvuma Juma Fuluge alieleza kuwa Mkoa wa Ruvuma ulipokea zaidi ya shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 448 katika shule za sekondari, vyumba vya madarasa 52 kwenye vituo shikizi pamoja na mabweni matatu 3 katika shule za sekondari.

Aliongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma una jumla ya shule za sekondari 214 pamoja na shule za msingi 818 ambapo mradi huu wa mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 umesaidia kupunguza changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa katika shuleza sekondari Mkoani Ruvuma kwa Zaidi ya asilimia 80%.

Amewarai  wakuu wa shule kuhakikisha wanasimamia na kutunza miundombinu ya madarasa yaliyojengwa pamoja na samani zake ili kuhakikisha inatumika kwa manufaa ya watoto watakaondelea na masomo katika shule hizo.

Ametoa wito kwa wananchi Mkoani Ruvuma kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa UVIKO 19 kwa kupata chanjo ya ugonjwa huo kwa hiyari. 

Mwisho. 

  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa