• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AZUNGUMZA NA KAMATI YA UTOAJI HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: July 29th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

29 JULAI 2022

Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda ameongoza kikao cha Kamati ya watoa huduma ya msaada wa kisheria Mkoani Ruvuma leo tarehe 29 Julai 2022.

Akizungumza katika kikao hicho, Pinda alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa sheria ya utoaji huduma ya msaada wa kisheria ni kuhakikisha inasaidia wananchi wanapata haki ya huduma ya kisheria bure pamoja na elimu ya sheria kwa ujumla.

Alibainisha kuwa Wizara ya Katiba na Sheria inaendelea kutengeneza mazingira ya upatikanaji haki na huduma ya msaada wa kisheria kwa kuondoa gharama za ada ya usajili wa usaidizi wa utoaji huduma ya msaada wa kisheria.

Aliongeza kuwa Serikali imeandaa mpango wa uandaaji wa vituo jumuishi vya sekta ya sheria ambavyo vitarahisisha utoaji wa huduma za kisheria kwa wananchi wote.

Pinda alisema kuwa katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Wizara imetenga fedha kwa ajili ya utoaji wa msaada wa kisheria ikiwemo kazi za bodi ya ushauri ya msaada wa kisheria.

Ametoa rai kwa wajumbe wa kamati hiyo kuzingatia na kutekeleza majukumu yao kama yalivyoainishwa katika muongozo wa uundaji wa kamati za Mkoa pamoja na kushirikiana na jamii katika kupinga unyanyasaji wa wanawake na watoto kwa kuhakikisha waathirika wanapata haki stahiki.

Amewasisitiza wadau wa sheria kuandaa vitabu vyenye sheria ndogondogo kwa kutumia lugha ya Kiswahili kwa lengo la kuwezesha jamii kuelewa sheria mbalimbali kwa urahisi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Mary Makondo alisema kuwa Sheria ya msaada wa kisheria ilipitishwa rasmi mwaka 2017 na 2018 ambapo hadi sasa ni takribani miaka 5 tangu imeanza kutumika nchini.

Alieleza kuwa lengo la Wizara ni kusimamia na kuratibu watoa huduma za msaada wa kisheria nchini kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo bure na kwa viwango vinavyotakiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Phillipo Beno  ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa kutoa elimu juu ya upatikanaji na utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria ambayo itawasaidia wananchi kupata haki zao pale inapohitajika.

Akiwakilisha wajumbe wa kamati ya utoaji huduma za msaada wa kisheria Mkoani Ruvuma, Shekhe Songambele ameipongeza Serikali kwa kutenga kitengo maalumu kinachotoa msaada wa kisheria kwa kuzingatia misingi ya kidini hasa katika kupambania haki za wanawake na watoto pamoja na mirathi.

 Mwisho. 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa