• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII AMEWATAKA WANANCHI KUHIFADHI NA KULINDA UTAMADUNI WETU.

Tarehe ya kuwekwa: February 27th, 2023

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mary  Massanja amewataka Wananchi kuwaenzi  viongozi wa mashujaa pamoja na kuhifadhi mila na tamaduni zetu ambazo yatupasa  kulinda, kuondoa uadui, ujinga, kupambana na ujangili  wa wanyama pori,  kupinga madawa ya kulevya pamoja na kupinga unyanyasaji wa kijinsia.

Amewataka kutumia na kutunza  kumbukumbu za kihistoria  ambazo zinaweza kutumika kuanzisha matamasha mbalimbali ambayo yatasaidia kuhifadhi  urithi wetu kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kingine pamoja upatikanaji wa fursa ya ajira ambazo zitaongeza kipato kwa jamii ikiwa maadhimisho hayo yataratibiwa vizuri.

Hayo yamejiri katika kilele cha maadhimisho ya  118  ya mashujaa wa vita vya majimaji ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 27 Februari  ya kila mwaka ambyo yalihudhuriwa na wadau mbalimbali wa maakumbusho wa mashujaa, Viongozi, na wanachi kwa lengo la kuwaenzi mashujaa waliojitoa mhanga katika kupigania, Haki, Uhuru na amani katika Taifa letu iliyofanyika katika uwanja wa mashujaa Songea.

Mhe. Mary alisema Serikali imekuwa ikipokea taarifa kuwa kuna mali kale ambazo zilichukuliwa ikiwemo na fuvu la Songea Mbano ambapo katika kutekeleza taarifa hiyo Serikali imeunda kamati ya kitaalamu  ya kuratibu kazi na kubaini mali kale zilizopo nje ya Nchi ili kuandaa mpango wa kurejesha na kuzifanya ziwe kumbukizi. “Alibainisha”.

Aliongeza kuwa Historia ya Tanzania haiwezi kukamilika bila kuwataja mashujaa wa vita vya majimaji ambao walijitoa uhai wao kwa kupinga uvamizi wa Tawala za kikoloni  ambapo Mashujaa hao walitumia mbinu za asili dhidi ya wakoloni waliokuwa na silaha Imara ambapo pamoja na kushindwa vita hivyo walipanda mbegu ya Utaifa, Uzalendo, Ukakamavu, Amani, na Upendo katika  Taifa Letu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,  Ndugu Kapenjama Ndile ambaye ni  Mkuu wa Wilaya ya Songea  alisema “Maadhimisho hayo yanatoa fursa kwa wadau kushiriki, kujadili, kutembelea na kuonesha vivutio vya  Utalii vilivyoko Tanzania hususani Mkoa wa Ruvuma.”

Ndile alibainisha kuwa maadhimisho hayo yalizinduliwa tarehe 25 Februari ambapo zilifanyika shughuli mbalimbali ikiwemo na mkesha wa shughuli za kitamaduni, burudani, maonesho ya vyakula vya asili, kufungua Ukumbi wa Historia, Uzinduzi wa uboreshaji wa Makumbusho ya Majimaji  baada na Kabla pamoja na kitabu cha Kihistoria  na mdahalo uliofanyika katika Wilaya ya Tunduru.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa ya Vita vya Majimaji Dkt. Noel Luoga  alisema baada ya  kupata Uhuru Baba wa Taifa kupitia kamati ya chama cha TANU 1965 alipitisha  azimio la kujenga Minara ya kudumu ya kumbu kumbu ya mashujaa wote katika maeneo ya Kihistoria ya chimbuko la kupigania Uhuru.

  Dkt. Luoga alibainisha kuwa,  katika kutekeleza azimio hilo Mamlaka ya Mkoa wa Ruvuma iliamua kujenga Makumbusho ya Majimaji  katika eneo ambalo walizikwa  Mashujaa 67 wa vita vya Majimaji  na baada ya kukamilika ujenzi  yalifunguliwa  rasmi na Baba wa Taifa Mwl Julius K. Nyerere tarehe 06 Julai 1980.

KAULI MBIU;

“MAKUMBUSHO YA MAJIMAJI NI URITHI WETU KWA MAENDELEO YA UCHUMI NA UTALII.”

                                                                                                   

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 







Matangazo

  • MATANGAZO mbalimbali ya Manispaa ya Songea kwa njia ya Redio January 31, 2020
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Januari 2020 January 25, 2020
  • MATANGAZO muhimu kwa wakazi wa Manispaa ya Songea January 31, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MIAKA MIWILI YA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN " SONGEA MC "

    March 17, 2023
  • BIL 145.77 KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI MJI WA SONGEA.

    March 11, 2023
  • YALIYOJIRI SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MKOANI RUVUMA

    March 09, 2023
  • DC Songea ameitaka Jamii kupinga Ukatili wa Kijinsia

    March 02, 2023
  • Tazama zote

Video

BIL. 145.77 KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI MJI WA SONGEA
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa