• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NI ZAIDI YA MIL. 100 ZAOKOLEWA NA TAKUKURU MKOANI RUVUMA KATIKA KIPINDI CHA JULAI-SEPTEMBA 2020.

Tarehe ya kuwekwa: October 23rd, 2020

Taasis ya kuzuia na kupambana na rushwa ( TAKUKURU) ni chombo kilichopewa dhamana kwa mujibu wa sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11, ya mwaka 2007 ya kuongoza vita dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Hamza Mwenda  katika kikao na Waandishi wa Habari  ambacho hufanyika kila baada ya robo ya mwaka ambapo husomwa taarifa ya  utendaji kazi na mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miezi mitatu kilichofanyika katika ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma 23 oktoba 2020.

Mwenda alisema  katika kipindi hicho TAKUKURU Mkoani Ruvuma ilipokea jumla ya taarifa 160 kutoka kwa wananchi kupitia vyanzo mbalimbali ambapo idara zilizolalamikiwa ni vyama vya siasa 35 (rushwa kwenye kura za maoni), Serikali za mitaa 24( watendaji wa kutosoma taarifa za mapato na matumizi na kufanya ubadhilifu wa fedha za vijiji), taasis za fedha 20, Ardhi 20, na polisi 11,   Elimu 7, mahakama 5, biashara 4, afya 4, misitu 4, mifungo 3, maji 2, madini 2, sheria 2, kilimo 3, ushirika 1, viwanda 1, usafirishaji 1, na   nishati 1.

Aliongeza kuwa  TAKUKURU Mkoani Ruvuma imefanya kazi ya uchambuzi wa mfumo wa ukusanyaji wa ushuru wa huduma (service leavy) Wilayani Namtumbo na Nyasa na kubaini Halmashauri kutokusanya Zaidi ya kiasi cha  shilingi milioni 36 kutoka kwa kampuni 18 zilizofanya kazi chini ya TARURA na TANROADS.

Aidha, TAKUKURU  Mkoani Ruvuma imefanya ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo nane “8”  yenye thamani ya bilioni 3 tatu kwa lengo la kujiridhisha iwapo fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo zinaendana na thamani halisi ya utekelezaji wa miradi katika sekta ya maji, barabara, na elimu ambayo ni mradi wa barabara  ya lami kilosa-bomani-ikulu mpya wilayani Nyasa   wenye thamani ya milioni 474,427,000, mradi wa RUWASA wenye thamani ya milioni 390,870,000.

 Mradi wa upanuzi na ukarabati wa mradi wa maji kijiji cha namasakata Wilayani Tunduru wenye thamani ya shilingi 147,154,975, mradi wa ujenzi wa madarasa matatu “3” shule ya msingi Mlingoti wenye thamani ya milioni 60,000,000, mradi wa ujenzi wa matundu 19 ya vyoo vya wanafunzi shule ya msingi mwenge Wilayani Namtumbo wenye thamani  shilingi milioni 28,517,086, mradi wa maji mtiririko Mkongo Gulioni-Nahimba wenye thamani ya shilingi milioni 2,069,575,521.

Akiitaja miradi mingine iliyofuatiliwa na TAKUKURU Mkoani Ruvuma ni ujenzi wa tanki la maji la Lusaka Mbinga Mjini lenye ujazo wa 500m3 lililogharimu shilingi 200,135,522,  pamoja na mradi wa wa maji kijiji cha Myangayanga Mbinga Mji wenye thamani ya shilingi 35,220,396.  “Mwenda alisema.”

Hata hivyo aliwaeleza waandishi wa Habari kuwa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma imeendelea kutekeleza jukumu la kushirikisha na kuelimisha jamii katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kufanya semina 69, mikutano ya hadhara 30, klabu 54 za wapinga rushwa mashuleni , Makala 2, redio 14 pamoja na Website za Halmashauri.

Mwisho, aliitaja mikakati waliyojiwekea kuelekea katika kipindi cha Kampeni za wagombea wa vyama vya siasa ni pamoja na kutoa elimu kwa  wananchi ili wafahamu umuhimu wa uchaguzi, lengo la uchaguzi, sheria zinazoongoza uchaguzi, umuhimu wa kupiga kura, na thamani ya kura.

Alimaliza kwa kutamka “Mapambano dhidi ya Rushwa ni jukumu letu wote”

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

 AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

23 OKTOBA 2020.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa