• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NMB yazipiga jeki shule mbili za sekondari Namtumbo

Tarehe ya kuwekwa: February 13th, 2019

BENKI ya NMB imechangia jumla ya viti 50 na meza 50  kwa ajili ya shule ya sekondari Narwi na kompyuta tano kwa ajili ya shule ya sekondari Rwinga zilizopo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma.

Hafla ya kukabidhi vifaa hivyo imefanyika katika shule ya sekondari ya Narwi ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo.

Akizungumza katika hafla hiyo Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Janeth Shango amesema  vifaa vyote vilivyotolewa katika shule hizo vimegharimu shilingi milioni tano.

“NMB tumeamua kushirikiana na shule hizi za Narwi na Rwinga ili kuwa jirani na jamii inayotuzunguka,kompyuta tulizozitoa katika shule ya sekondari ya Rwinga  zitasaidia kuimarisha somo la TEHAMA’’,alisema Shango.

Hata hivyo Meneja huyo wa NMB Kanda  ya Kusini amesema Benki hiyo imekuwa inapokea maombi mengi ya kuchangia  miradi ya jamii na kwamba NMB imejikita zaidi katika maeneo ya elimu,afya na misaada ya hali na mali katika nyakati ngumu za majanga.

Kulingana na Shango,Katika kipindi cha mwaka 2018,NMB ilitenga zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya jamii hali iliyosababisha Benki hiyo kuwa ya kwanza kuchangia maendeleo kuliko benki yoyote nchini.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika hafla hiyo,Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo ameishukuru na kuipongeza Benki ya NMB kwa kuwajali wateja wake hali ambayo inadhihirisha kwa vitendo kuwa Benki hiyo ipo jirani ya jamii.

“Katika wilaya yetu ya Namtumbo karibu watumishi wote,fedha za tumbaku,korosho na mazao mengine yote,fedha zao zinapitia Benki ya NMB kutokana na huduma bora zinazotolewa na Benki hiyo’’,alisema Kizigo.

Amesema licha ya msaada wa madawati na kompyuta walizotoa,NMB pia wamekuwa wanachangia huduma mbalimbali za elimu na afya katika wilaya hiyo ikiwemo mradi wa ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Namtumbo ambayo Benki hiyo imekuwa inachangia kila mwaka katika hatua za mradi huo.

Hata hivyo Kizigo amesema wilaya hiyo inaanzisha kampeni mpya kuanzia mwaka huu ya  ujenzi wa mabweni katika shule zote 30 za sekondari za serikali,hivyo ametoa rai kwa uongozi wa NMB kuendelea kuichangia miradi hiyo itakapoanza kutekelezwa.

Awali Mkuu wa Shule ya sekondari ya Narwi, Monica Kayombo  akitoa taarifa kabla ya kukabidhiwa  viti na meza 100,ameishukuru Benki ya NMB kwa msaada huo ambao amesema umepunguza changamoto ya madawati katika shule hiyo.

Kayombo amesema shule hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 2009 ina wanafunzi 404 wanaosoma kidato cha kwanza hadi cha nne na kwamba shule hiyo ina  meza na viti 200 kati ya 404 zinazohitajika na kwamba shule ina madawati 48 huku upungufu ukiwa ni madawati 108.

Naye Mkuu wa shule ya sekondari ya Rwinga Suleiman Mohamed Alawi ameishukuru Benki ya NMB kwa msaada wa kompyuta tano ambazo amesema zitasaidia kutatua changamoto ya gharama kubwa ya uchapaji wa mitihani ya ndani ya shule na mitihani ya ujirani mwema.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Dani Nyambo  amesema anatambua mchango mkubwa unaofanywa na Benki ya NMB katika wilaya hiyo na kusisitiza kuwa mchango wa viti na meza 100 na kompyuta tano utasaidia wanafunzi kuimarika katika teknolojia ya habari na mawasiliano ambayo imeifanya dunia kuwa kijiji kimoja.

Yusufu Mwambe ni Diwani wa Kata ya Rwinga ambaye shule mbili za Narwi na Rwinga zilizopo katika Kata yake zimefaidika na msaada wa Benki ya NMB,ameshukuru kwa niaba ya wananchi na wanafunzi wa kata hiyo kwa msaada mkubwa ambao umepunguza changamoto zilizokuwa zinazikabili shule hizo.

“NMB wanafanya biashara hivyo kusema tu ahsante kwa maneno haitoshi,nawaomba wananchi wote wa kata yangu na watanzania kwa ujumla tuseme ahsante kwa kufungua akaunti katika Benki ya NMB’’,alisisitiza Mwambe.

NMB ndiyo  Benki inayoongoza nchini kwa kufika wilaya zote nchini kwa asilimia 100,ina matawi zaidi ya 228,ATM zaidi ya 800,wakala wa NMB zaidi ya 6,000 na idadi ya wateja zaidi ya milioni tatu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

Februari 13,2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa