• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Nufaika na huduma za Uwekezaji wa Masoko ya Fedha.

Tarehe ya kuwekwa: November 13th, 2020

 Benki kuu ya Tanzania( BOT)  kwa niaba ya Serikali zote mbili yaani  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar huuza Dhamana za Serikali ikiwa ni njia ya kukopa fedha kutoka kwa taasisi mbalimbali na mwananchi mmoja mmoja.

Kauli  hiyo imetolewa na kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Jeremiah E. Sendoro akiwakilishwa na Afisa Kilimo Mkoa wa Ruvuma Enock Ndunguru katika semina ya uwekezaji katika masoko ya fedha iliyotolewa na Benk kuu ya Tanzania (BOT)  iliyo shirikisha watumishi wa umma, wadau wa taasis za fedha, na wananchi mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa Songea Club tarehe 11 Novemba 2020.

 Naye mwezeshaji  kutoka Benki Kuu ya Tanzania ( Dar es saalam) Fidelis Mkatte  alisema “Dhamana za Serikali za muda mrefu ni dhamana zinazoiva katika muda unaozidi mwaka mmoja, hata hivyo  dhamana hizo  za Serikali za muda mrefu kwa kiwango kikubwa huiwezesha Serikali kugharamia kwa muda nakisi katika bajeti yake inayosababishwa na upungufu wa mapato ukilinganisha na matumizi ya Serikali”.

Dhamana hizo huuzwa kwenye soko la awali kwa njia ya ushindani kupitia minada na baada ya hapo uuzaji wa dhamana hizo hufanywa kwenye soko la upili. Pia kiwango cha chini cha kuwekeza kwenye dhamana za Serikali za muda mrefu ni shilingi milioni moja 1,000,000 zikiwa katika mafungu ya shilingi laki mojamoja 100,000.

Aidha, Mpango huu hutolewa kupitia kwenye magazeti na hupatikana  kwenye tovuti ya Benk kuu ya Tanzania; www.bot.go.tz, ukiwa unaonyesha dhamana ya Serikali itakayotolewa na tarehe yam nada.

 Faida kwa mwekezaji ni  Kuwekeza katika dhamana za Serikali ambazo ni salama kwani Serikali haitarajiwi kukiuka mategemeo ya wadai wake wakati wa malipo,  Dhamana za Serikali zinahamishika, hivyo mwekezaji anaweza kuziuza kabla ya muda wake wa kuiva endapo itakuwa ni lazima afanye hivyo.  Dhamana za Serikali zinaweza kutolewa kama dhamana kwa ajili ya mkopo pamoja na  dhamana za Serikali kuwa na  kiwango cha faida inayoridhisha”.

Akizita faida kwa upande wa Serikali ni Kugharamikia upungufu wa kibajeti (T-bills),  Kupata fedha za kuendesha Miradi ya Maendeleo (T-bonds), Kusimamia Ujazo wa Fedha katika Uchumi, pamoja na  kusaidia kusimamia mfumuko wa bei.

Aliwaasa  walishiriki wa mafunzo hayo kuanza  kuwekeza  fedha zao katika masoko ya fedha ili waweze kunufaika na huduma hizo kwa kwenda tawi lolote la Benki kama CRDB na atapewa fomu ya maelekezo ya taratibu zote za uwekezaji wa masoko ya fedha ambapo  kima cha chini ni tzs 500,000 kwa dhamana za muda mfupi na tzs 1,000,000 kwa dhamana za muda mrefu .

Alifafanua katika  kuandaa muungozo huo, mambo yafuatayo yalizingatiwa ikiwemo na  Dhamana zinazoiva, Ukopaji mpya, na  Malengo katika kusimamia ujazo wa fedha kwenye mzunguko.  Alisema  “ KODI YA ZUIO”  kwa Wawekezaji katika Dhamana za Serikali za Muda Mfupi pamoja na Dhamana za Serikali za Miaka 2 hulipa kodi ya zuio (10%) katika mapato yatokanayo na uwekezaji wao.

 Wawekezaji katika Dhamna za Serikali za Miaka 5, 7, 10, 15 na 20 hawalipi kodi ya zuio. Hii ni katika kuhamisisha uwekezaji katika Dhamana za Serikali kwa  Muda Mrefu ambazo huwa bora Zaidi kwa Serikali (Mkopaji). Alisisitiza Mkatte.

Dhamana zinazoiva,  hulipwa kwa kutumia Dhamana zinazotolewa upya, na kiwango kinachopatika Zaidi ya mahitaji ya kulipa Dhamana zinazoiva huhesabika kama ukopaji mpya. Pia ingawa gharama za kulipia Dhamana zinazoiva hutokana na ukopaji mpya, faida wanayostahili kulipwa wawekezaji hulipwa kutokana na mapato ya ndani ya Serikali.

Mwisho alisema,  Uwepo wa Dhamana za Serikali imekuwa chachu kubwa katika kufanikisha malengo mbalimbali ya serikali ikiwemo na Benki Kuu kufanikiwa kusimamia mfumuko wa bei, Serikali kufanikiwa kukopa kwa gharama nafuu katika riba za soko (competitive rates) na kupata fedha kwa ajili ya mahitaji mbalimbali ya ki-bajeti  pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa jamii.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;                                                                                                                                     

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

13 Novemba 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa