• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NYONGEZA YA MKATABA WA LISHE KUSAINIWA MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: December 2nd, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

02.12.2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imesaini nyongeza ya mkataba wa utendaji kazi na usimamizi wa shughuli za lishe kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia tarehe 01 Julai 2021 hadi tarehe 30 Juni 2026 kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya utapiamlo katika jamii.

Mkataba huo umesainiwa leo tarehe 02 Disemba 2021 na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea pamoja na watendaji wa kata ambao ni watekelezaji wa mkataba huo katika ngazi ya jamii, ambapo zoezi hilo limefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Zoezi hilo limefanyika ikiwa ni katika utekelezaji wa kauli iliyotolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassani mnamo mwaka 2017 kutokana na kukithiri kwa hali duni ya lishe na udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 nchini ambapo aliagiza kuwepo kwa mkataba wa usimamiaji wa utekelezaji wa shughuli za lishe kati ya ofisi ya Makamu wa Rais na wakuu wa Mikoa yote 26 ndani ya Tanzania bara.

Akibainisha lengo la kusaini mkataba huo, Mgema alisema kuwa mnamo tarehe 24 Septemba 2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma iliingia mkataba wa utendaji kazi na usimamizi wa shughuli za lishe na Wakuu wa Wilaya zote 5 zilizopo ndani ya Mkoa wa Ruvuma ambapo mkataba huo umekuwa ukitekelezwa kwa muda wa miaka mitatu kuanzia tarehe 25 Septemba 2018 hadi tarehe 30 Juni 2021.

Mgema aliongeza kuwa tangu kusainiwa kwa mkataba huo ,ofisi ya Mkuu wa Mkoa na wadau wengine wa lishe walifanya tathimini sita na kubaini kuwa shughuli za lishe ni mtambuka na endelevu ambapo utekelezaji wa mkataba huo ulisaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la utapiamlo katika jamii.

Alisema kuwa kwa kuzingatia umuhimu na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa awamu ya kwanza, pande zote mbili zilikubaliana kuongeza muda wa utekelezaji wa mkataba huo kwa sababu hakutakuwa na mabadiliko makubwa kwenye maeneo mahususi yanayotekelezwa na mamlaka ya Serikali za mitaa na hivyo kutoathiri viashiria vingi katika mkataba wa lishe wa awali.

Kwa upande wake Afisa lishe Manispaa ya Songea Florentine Kissaka amewataka watendaji wa kata kuhakikisha wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa nyongeza ya muda wa mkataba wa lishe katika ngazi ya jamii ili kuhakikisha elimu ya lishe inamfikia kila mwananchi na hatimaye kuondoa kabisa changamoto ya udumavu na utapiamlo.

Kissaka alibainisha kuwa katika kipindi cha Julai-Septemba 2021 hali ya utapiamlo na udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano imefikia kiwango cha asilimia 0.1% ambapo miongoni mwa yaliyochangia kushuka kwa kiwango cha watoto wenye utapiamlo ndani ya Manispaa ya Songea katika utekelezaji wa mkataba wa lishe ni pamoja na usimamizi mzuri wa viongozi kuanzia ngazi ya Wilaya, Halmashauri, kata na mitaa.

Aliongeza kuwa miongoni mwa changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa awamu ya kwanza ni pamoja na kiwango kidogo cha utambuzi wa watoto wenye utapiamlo katika jamii na baadhi ya kata kuchelewa kuleta taarifa ya utekelezaji wa mkataba katika maeneo yao kwa wakati.

Ametoa wito kwa watendaji wa kata kuongeza wigo wa kufanya uchunguzi wa hali ya lishe ili kuweza kuibua watoto wengi Zaidi wenye tatizo la udumavu na utapiamlo pamoja na Halmashauri kutoa motisha kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili kuimarisha usimamizi kwenye ngazi ya kata na mitaa ambako ndiyo kiini cha kuleta mabadiliko katika jamii.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa