• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NYOTA iliyochomoka toka Sayari ya Jupiter imeangukia kusini

Tarehe ya kuwekwa: May 11th, 2018

SERIKALI imedhamiria kuitumia nyotamkia(kimondo) iliyoanguka katika Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe kuutangaza utalii wa Tanzania baada ya kubainika kivutio hicho ni adimu duniani.

Moja vivutio adimu vya utalii vinavyowashangaza wengi  ni nyotamkia (kimondo) ambayo iliyochomoka toka Sayari ya Jupiter mwaka na kuanguka mwaka 1840 katika kijiji cha Ndolezi Wilaya ya Mbozi ni moja ya kivutio kinachowashangaza wengi.

Nyotamkia hiyo ina uzito wa tani 12 ikiwa ni ya nane kwa ukubwa duniani kati ya nyotamkia  zaidi ya 600 zilizoanguka toka angani sehemu mbalimbali ulimwenguni.

Utafiti unaonesha kuwa nyotamkia hiyo inaongoza kwa ubora ukilinganisha na nyotamkia zilizoanguka sehemu mbalimbali duniani.Nyotamkia au kimondo cha Mbozi kina madini ya chuma kwa zaidi ya asilimia 90.

Nyotamkia ya Mbozi katika historia ya nyotamkia zilizoanguka duniani haikubahatika kushuhudiwa na mtu yeyote wakati inashuka toka kwenye obiti yake angani kuja duniani mwaka 1840.

Hata hivyo kinachowavutia wengi ni kwamba nyotamkia hii ilikuja kuonekana tayari ikiwa imeanguka chini wakati wa utawala wa Mjerumani mwaka 1930 ambapo watalaamu wa kijerumani  mwaka 1931 walikata kipande cha nyotamkia hiyo na  kukipeleka nchini Ujerumani ili kukifanyia utafiti.

Mhifadhi Kiongozi wa Makumbusho ya Taifa Philipo Maligissu anasema nyotamkia hiyo baada ya kupimwa ilionesha ina urefu wa mita tatu,unene wa mita 1.12,upana mita moja,ina uzito wa tani 12, nyotamkia hiyo iligundulika kuwa  na aina tano za madini mbalimbali huku sehemu kubwa yakiwa ni madini ya chuma.

Anayataja madini yaliyomo katika nyotamkia hiyo kuwa  ni chuma kipo kwa asilimia 90.45,madini ya nikel asilimia 8.66, shaba asilimia 0.69,sulfa asilimia 0.11 na  madini ya fosiforasi ni asilimia 0.11.

“inaaminika kuwa nyotamkia ya Mbozi ndiyo ya kwanza kwa ubora duniani ukilinganisha na nyotamkia nyingine zilizoanguka duniani ambazo asilimia kubwa ni  mawe na uzito wa kuanzia kilo tano  tu’’,anasisitiza Maligisu.

Utafiti umebaini nyotamkia ya Mbozi ndiye pekee yenye madini ya aina tano wakati nyotamkia nyingine ikiwemo iliyoanguka nchini Afrika ya kusini ina uzito wa tani 60 na ya nchini Uingereza ina tani 30 lakini nyota hizo hazina ubora wowote wala madini,zaidi ya kuwa ni mfano wa jiwe linalopasuka kirahisi hali ambayo inasababisha watalii kutoka kona zote  kutembelea zaidi nyotamkia ya  Mbozi.

Makala hii imeandaliwa na 

Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 11,2018

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa