• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

OCEAN ROAD kupandikiza matiti wagonjwa wa saratani

Tarehe ya kuwekwa: September 2nd, 2018

WANAWAKE waliopoteza matiti kutokana na kuugua saratani, watafanyiwa upasuaji wa kibingwa wa kurudishia tena kiungo hicho.

Upasuaji huo unaojulikana kitaalamu kama ‘Breast reconstruction after mastectomy’ utafanywa katika Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI).

ORCI ipo katika maandalizi ya kufikia hatua hiyo ya upasuaji wa kibingwa ikiwa ni moja kati ya makubaliano ya ushirikiano na Taasisi ya Saratani ya China (Chinese Academy of Medical Science – Cancer Hospital (CAMS – CH)).

Makubaliano hayo yalisainiwa hivi karibuni mjini Beijing, China na Mkurugenzi wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage na Mkurugenzi wa CAMS – CH, Dk. Jie He, yalishuhudiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

Dk. Mwaiselage alisema saratani ya matiti ni miongoni mwa saratani zinaozoongoza kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wanaopokewa na kuhudumiwa hospitalini hapo.

“Hivyo, tutashirikiana na wataalamu wenzetu kutoka katika taasisi hiyo upande wa upasuaji wa saratani hii. Ikigundulika mapema si lazima kutoa titi lote, tunaweza kutoa ule uvimbe uliopo pale na kuacha titi, lakini lazima uwe na mashine za kisasa za kutoa tiba mionzi (LINAC) ambazo tayari tunazo.

“Hata tukilitoa titi lote, tunatoa kutokana na upasuaji ambao unakuwa ni bora zaidi katika utoaji wa tiba hiyo, lakini baada ya upasuaji huo wa kuliondoa titi, kuna upasuaji unaofuata ‘breast reconstruction surgery’ (tiba ya kupandikiza titi).

“Kupitia makubaliano ya ushirikiano huu, tunakusudia wataalamu wa taasisi hiyo waje nchini ili kuwajengea uwezo wataalamu wetu wa ndani, jinsi gani ya kutoa huduma hiyo kwa usahihi,” alisema.

Alisema titi ni kiungo muhimu kwa mwanamke na linapotolewa humwathiri kisaikolojia na sasa kupitia makubaliano hayo wataanza kutoa huduma hiyo.

Dk. Mwaiselage alisema pia kutakuwa na mafunzo ya juu kwa madaktari bingwa wa saratani (super specialization).

Kwamba wataalamu kutoka China watakuwa wakija nchini kuwafundisha kwa vitendo wataalamu wa ndani kwa kila saratani husika hasa zile zinazoongoza nchini.

Alisema wamekubaliana pia taasisi hiyo itoe mafunzo ya muda mrefu kwani Tanzania inakabiliwa na upungufu wa madaktari bingwa, hasa kwa upande wa magonjwa ya saratani kwa upasuaji.

“Lakini kwa kuwa ORCI hatufanyi upasuaji, tumelenga kwamba madaktari watakaokwenda kujifunza mafunzo hayo watatoka Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas-Mloganzila),” alisema.

Alisema pia wamekubaliana kufanya tafiti kwa pamoja na wamelenga zitasaidia katika kuimarisha huduma za kinga na tiba dhidi ya magonjwa hayo.

CHANZO NI MTANZANIA

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa