• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

OFISI za vijiji 12 Songea zapigwa jeki msaada wa mbao za matangazo

Tarehe ya kuwekwa: July 29th, 2018

OFISI za vijiji 12 wilayani Songea mkoani Ruvuma zimenufaika na msaada wa mbao za matangazo kwa ajili ya kubandika matangazo na taarifa mbalimbali ikiwemo ya mapato na matumizi pamoja na miradi ya maendeleo kwa lengo la kuongeza uwazi katika ngazi za vijiji wanavyofanyia kazi.

Msaada huo ulitolewa mwishoni mwa wiki na mkurugenzi mkuu wa asasi isiyo ya kiserikali ya Millenium Arts Group Mnung'a Shaib Mnung'a kupitia ufadhili wa The Foundation For Civil Society(FCS)ya Jijini Dar es salaam kwenye kongamano la ushawishi na utetezi juu ya masuala ya utawala Bora lililofanyika katika kata ya Magagura wilayani humo.

Mnung'a alivitaja vijiji vilivyonufaika na msaada wa mbao hizo za matangazo kutoka katika kata nne ambazo zimepitiwa na mradi wa utawala Bora kuwa ni Lusonga,Masangu,Kizuka,Magagura,Mbilo,Ngahokola,Litapwasi,Uyahudini,Lihangweni,Lipaya,Mpitimbi A na Mpitimbi B vyote vya wilayani Songea

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa wenyeviti wa vijiji hivyo,mkurugenzi huyo aliwataka viongozi hao kutumia mbao hizo za matangazo kwa ajili ya kubandika matangazo na taarifa mbalimbali za mapato na matumizi kwa ajili ya kuondoa manung'uniko na migogoro baina ya viongozi na wananchi.

Aidha amewataka wenyeviti hao kuzingatia misingi ya utawala Bora ikiwa pamoja na uwajibikaji,uwazi na ushirikishwaji wa wananchi katika kupanga,kutekeleza na kufanya ufuatiliaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa madai kuwa kuto kufanya hivyo kutapelekea wananchi kutokuwa na Imani na viongozi wao na kuwavunja moyo wa kujitolea katika shughuli za maendeleo.

Alisema kuwa miradi mingi ya maendeleo vijijini inakwama na mingine kutekelezwa chini ya kiwango kutokana na baadhi ya wenyeviti wa vijiji na watendaji wa kata kutoshirikisha wananchi na matokeo yake huzuka migogoro na malumbano kati ya viongozi na wananchi jambo ambalo linapelekea kukwamisha shughuli za maendeleo.

Akiongea kwa niaba ya wenyeviti wenzake,mwenyekiti wa kijiji cha Ngahokola wilayani Songea Eneck Haule ameipongeza na kuishukuru asasi hiyo kwa kutoa msaada huo kwa madai kuwa awali ofisi nyingi za vijiji hazikuwa na mbao hizo jambo ambalo litasaidia  kwa kiasi kikubwa kupunguza mahojiano toka kwa wananchi na kuamsha hali ya kujitolea.

Mwandishi ni Julius Konala wa Songea



















Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa