• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

PROF. JOYCE NDALICHAKO "Amewataka Maafisa Ustawi wa jamii kukusanya Takwimu sahihi za watu wenye Ualbino"

Tarehe ya kuwekwa: June 14th, 2023

Katika kipindi cha mwaka 2022/2023 Serikali ilitenga  bajeti ya  shilingi Mil. 50 kwa ajili ya kuboresha huduma za utoaji wa mafuta  kinga kwa watu wenye ualbino nchini.

Utekelezaji wa huduma mbalimbali nchini   umezingatia Sera, Mikataba ya kikanda, na kimataifa na Mipango mbalimbali ya nchi ikiwemo na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ilani ya Chama cha Mapinduzi pamoja na Sera ya Taifa ya huduma na maendeleo kwa watu wenye ulemavu, sheria ya watu wenye ulemavu  namba 9 ya mwaka 2010, na Mkataba wa Kimataifa wa watu wenye ulemavu 2006.

Aidha, Serikali inaendelea kuhimiza Halmashauri zote nchini kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kinga pamoja na kuongeza wataalamu  kwa  lengo la kudhibiti  saratani ya ngozi kwa watu wenye Ualbino.

Hayo yamejili katika kuadhimisha kilele cha Siku ya Kimataifa ya uelewa kuhusu Albino iliyofanyika kuanzia tarehe 11 juni hadi 13 juni 2023 Mkoani Ruvuma katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi wa kitaifa pamoja na wadau mbalimbali kwa lengo la kutoa uelewa kuhusu Albino.

Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, kazi, Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Prof Joyce Ndalichako (MB)  ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanal. Laban Thomas.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Songea Wilman Kapenjama Ndile kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma “ Amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii kuhakikisha wanapata takwimu sahihi kwenye maeneo yao za watu wenye Ualbino kwa ajili ya kutoa huduma muhimu.”

Ndile aliongeza kuwa, katika kuimarisha juhudi mbalimbali za ustawi wa jamii  kwa watu wenye ulemavu Serikali imechukua hatua za kuwawezesha walemavu kiuchumi pia kwa  kutambua juhudi za Serikali katika kushughulikia masuala ya watu wenye ulemavu.  “Alibainisha”

“ Serikali inachukua hatua mbalimbali katika kutekeleza matakwa ya kisheria ya watu wenye ulemavu kwa kupitia  utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020/2025.”

Amewataka kutoa ushirikiano, kujenga upendo na kufanya kazi kwa pamoja  ili kuepuka migogoro inayoweza kuleta chuki au kusambaratisha umoja na kuendelea  kuchangamkia fursa adhimu ili kujikwamua kiuchumi kwa kufanya marejesho  ya mikopo ili kutoa fursa kwa wengine  waweze kunufaika.

Alibainisha kuwa Ajira kwa watu wenye ulemavu imesimamia Takwa la 3% kuajiri  watu wasiopungua  20 ambapo katika kipindi cha mwaka 2023 Serikali imeajiri watumishi 812 na Intenalship 178.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Vyama vya Walemavu Tanzania ( SHIVYAWATA) Ernest Simaya  alisema “ Maadhimisho hayo yalianza mwaka 2006 na hatimaye kuungwa mkono na Mataifa  mbalimbali. 

Simaya alisema mambo ya msingi ambayo huyashughulikia ni pamoja na suala la ajira kwa walemavu ambapo kwa mwaka 2021/2022 Serikali imeajiri watumishi walimu ( walemavu) 245. “Alibainisha.”

Imeandaliwa na;                                                                        

Amina  Pilly;

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.   

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa