• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAIS WA TUCTA ASIMAMIA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA CHAMA CHA TALGWU MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: June 28th, 2021

Chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) ni chama kinachoundwa na wafanyakazi/Wanachama  kutoka katika Halmashauri za Majiji na Idara zake, Halmashauri za Manispaa na Idara zake, Halmashauri za Wilaya na Idara zake, mashirika ya maendeleo ya Uchumi, Mifuko ya Pensheni (PSSSF)  na mamlaka nyingine zingine za ajira. Ambapo wanachama wa TALGWU toka mamlaka hizo hulindwa na kutetewa maslahi yao kwa mujibu wa kanuni za Nchi.

Hayo yametamkwa na Katibu wa TALGWU Mkoa wa Ruvuma Ashraffu Chussi kwenye  mkutano wa TALGWU Mkoa wa Ruvuma uliofanyika tarehe 26 juni 2021 katika ukumbi wa AJUCO Manispaa ya Songea na kuhudhuliwa na Mh. Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), wajumbe  zaidi ya  237  kutoka kwenye  matawi 79  Mkoani Ruvuma, viongozi mbalimbali ngazi ya mkoa,  pamoja na Msimamizi wa Uchaguzi kutoka Idara ya Kazi Mkoa wa Njombe  kwa lengo la kufanya  chaguzi  za vingozi ngazi Mkoa na wawakilishi Mkutano mkuu Taifa.

Chussi alisema Katiba ya Chama cha TALGWU toleo la 2016 Ibara ya 5.10 inayoelekeza kufanyika kwa Mkutano Mkuu  kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa za kazi kwa kipindi cha miaka (5) 2016-2021 na kufanyika chaguzi za viongozi wa nafasi mbalimbali ambapo siku ya pili 27 juni 2021  baada ya uchaguzi kufanyika wajumbe wote  walipata semina ya utawala bora, na matumizi ya fedha za Chama.

Alisema TALGWU Mkoa wa Ruvuma ina wanachama 2859 kati ya watumishi wasio walimu  3792 sawa na 75% ya watumishi wote wasio walimu katika mkoa wa Ruvuma. Akizitaja changamoto zinazowakabili wanachama Mkoani Ruvuma ni pamoja na watumishi kutolipwa madeni ya uhamisho, likizo, matibabu na malimbikizo ya mishahara,  Wakurugenzi  Halmashauri kuhamisha watumishi bila kuwalipa stahiki zao kwa wakati kinyume na maelekezo ya serikali yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais, uchache wa watumishi sekta mbalimbali hasa Idara ya Afya pamoja na upungufu wa Vitendea kazi.

Mgeni Rasmi katika mkutano huo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Generali Wilbert Ibuge ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ambaye alisema “kazi ya kiongozi ni  kuonyesha njia, kutatua changamoto au kero za wanachama wake, kuwa wabunifu wa miradi ya maendeleo na kujiepusha na tamaa za fedha kwa maslahi ya chama”.

Pololet  alisema, Awali vyama vya wafanyakazi vilikuwa na migomo mbalimbali katika kudai haki lakini kwa sasa vyama vya wafanyakazi  wamekuja na utaratibu mpya wakutumia njia ya majadiliano na kukubaliana  jambo kwa pamoja.  Alisema  hiyo ndiyo njia sahihi.

Akijibu Risala iliyosomwa na katibu wa chama hicho ambapo alisema Serikali imefanya mambo mengi sana  na inaendelea  kuboresha  mazingira wezeshi kwa watumishi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi  pamoja kuongeza vitendea kazi kwenye vituo vya afya, vifaa tiba, dawa na vitenganishi vinatolewa kwa asilimia 98%.

Alibainisha kuwa kwa muda wa  miaka 5 iliyopita  Serikali imeanza kuboresha miundombinu ya afya Mkoani Ruvuma ambapo alisema vituo vya vya afya 15 na vingine vinajengwa ikiwemo na Halmashauri ya Nyasa  kituo 1, Halmashauri ya wilaya ya Songea 1, na halamashuri ya wilaya ya Namtumbo vimekamilika na kutoa huduma ya awali ya OPD na baada ya kupokea vifaa  huduma zote zitatolewa ikiwemo na upasuaji.

Aliongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma umepokea milioni 500 kwa kila Hospitali kwa ajili ya kuongeza WOD za wanawake, wanaume na watoto. Pia Halmashauri ya Wilaya ya Songea  imepokea  shilingi milioni  900  kwa ajili ya kujenga vituo 2 vya afya  Madaba na Mtyangimbole, pia Manispaa ya Songea imepokea  shilingi milioni 500 kwa ajili ya kituo cha afya Ruvuma, Shilingi  milioni 400 Magagura, na  shilingi  milioni 400 Matimila.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote na makatibu Tawala wa Mikoa wahakikishe wanalipa madai ya likizo, uhamisho, malimbikizo  kwa watumishi ambao wanadai na hadi kufikia ocktoba 30 2021 yawe yamelipwa.    Alisema  “Rais wa Nchi hii akiagiza hiyo ni sheria. Hata nyie watumishi mna haki ya kukataa kuhama kituo kimoja kwenda kituo kingine kama hujalipwa haki yako lakini mkizungumza kimahusiano hukatazwi”.  Pololet alisisitiza.

Naye Rais wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi (TUCTA) ambaye pia ni Mwenyekiti wa TALGWU Taifa Tumaini  Nyamhokya alisema wapo watumishi wanaolipwa mishahara kwa mapato ya ndani ambapo mishahara hiyo hulipwa bila kupeleka makato kwenye mifuko  husika  ambapo amewataka Waajiri wote kuhakikisha wanapeleka makato TRA, Mifuko ya jamii, mfuko wa TALGWU, pamoja  na  mfuko wa afya.

Mh. Rais Nyamhokya alisema miongoni mwa  mafanikio ya  chama kwa kushirikiana na TUCTA ni pamoja na kuwarudisha watumishi  zaidi 8000 hususani  wa darasa la 7  ambao  waliondolewa kazini pamoja na kurudisha kikokotoo  cha awali, na kupandisha madaraja kwa watumishi ambapo kuanzia julai 2021 kutakuwa na mabadiliko ya mishshara. Pia amewataka watumishi kuwa waaminifu kazini hususani wakusanyaji wa mapato ya ndani kwa kutumia POS.

 Naye Afisa kazi ambaye  alikuwa Msimamizi wa Uchaguzi Albert Luka Ngendelo alisema utaratibu wa kupiga kura utafuata kanuni za Chama toleo la 2018, kanuni ya kwanza, kanuni ndogo ya 6 katika kifungu kidogo cha 6 inayozungumzia uchaguzi wowote wa chama utafanyika kwa kupiga kura ya siri. pia kanuni ndogo ya kwanza  kanuni  ndogo ya 7 aya ya 5  ambayo inasema uchaguzi wa kujaza nafasi nyingi za makundi,  ushindi utahesabiwa kwa kupata wingi wa kura alizozipata muombaji kwa mujibu wa katiba.

Mwisho, Ngendelo alitangaza matokeo ya uchaguzi wa nafasi mbalimbali za uongozi kwa wagombea ambapo ngazi ya Mwenyekiti Mkoa mgombea alikuwa mmoja ambaye ni Wily Luambano  ambaye alipigiwa kura za ndiyo/hapana ikiwa kura zilizopigwa ni 229, kura zilizoharibika 8, kura za hapana 27, na kura za ndiyo ni 194 kisha kumtangaza  ndugu Wily David Luambano kuwa Mwenyekiti wa TALGWU Mkoa wa Ruvuma.

                             TALGWU CHAMA IMARA HUDUMA BORA KWA WANACHAMA

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

28 JUNI 2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa