• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC IBUGE " AJIPANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA MKOANI RUVUMA".

Tarehe ya kuwekwa: December 21st, 2021

Na;

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

21 DISEMBA 2021.

Mkoa wa Ruvuma wajipanga kukabiliana na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara wa sekta binafsi na umma kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Generali Brigedia Balozi Wilbert Ibuge katika baraza la wafanyabiashara Mkoani Ruvuma, lilifonyanyika leo tarehe 21 Desemba 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wafanyabiashara.

Ibuge alisema kuwa baraza la wafanyabiashara la Mkoa wa Ruvuma limefanyika kwa mujibu wa sheria kupitia waraka namba 1 wa mwaka 2001 uliotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao unaelekeza kufanyika kwa mabaraza  kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa kwa lengo la kujadiliana changamoto zinazowakabili wafanyabiashara pamoja na utatuzi.

Ameongeza kuwa baraza hilo linatoa fursa kwa sekta binafsi na umma kujadili kwa pamoja changamoto zinazowakabili na kuzitatua  kwa lengo la kukuza uchumi kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Ametoa wito kwa Taasisi binafsi kutumia fursa za kibiashara zilizopo ndani ya Mkoa wa Ruvuma katika uwekezaji, ambapo miongoni mwa fursa hizo ni pamoja na uchakataji wa asali, utalii, uvuvi, mifugo na kilimo.

Amezitaka Taasisi za Serikali kutoa huduma kwa wafanyabiashara ikiwemo na utoaji wa leseni na vitambulisho, kuboresha mazingira rafiki kwa wafanyabiashara ikiwemo na miundombinu ya barabara pamoja na kuandaa maeneo stahiki ya kufanyia biashara kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kuleta uchumi jumuishi kwa manufaa ya wananchi wote kwa ujumla.

Naye Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Biashara (TMBC) Dr. Godwill Wange amesema kuwa miongoni mwa maazimio yaliyowekwa katika baraza hilo ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya msingi ili kufanikisha mazingira stahiki ya biashara hasa kwa wajasiriamalli (machinga), pamoja na Taasisi za uthibiti wa mazingira na OSHA kuhakikisha wana wawakilishi katika kila Wilaya Mkoani Ruvuma kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara.

Amesema kuwa wawekezaji wote wanatakiwa kushirikiana  kwa pamoja na kuzitumia fursa za kibiashara ambazo bado hazijafunguka ili kujenga viwanda ambavyo vitatumika kutengeneza bidhaa zinazotokana na rasimali zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma.

Wange amewataka viongozi wa baraza la Wilaya kuhakikisha wanatatua changamoto za wafanyabiashara kabla ya kuzipeleka ngazi ya Mkoa  kwa lengo la kurahisisha utatuaji wa changamoto hizo kwa wakati.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Wakuu wa Wilaya 5, Wakurugenzi wa Halmashauri 8 pamoja na viongozi mbalimbali kwa kuweza kusimamia vizuri utekelezaji wa miradi ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19  kabla ya wakati uliopangwa na Serikali.

Oddo amewataka viongozi kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhesabiwa katika sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwaka 2022 nchi nzima kwa lengo la kupata Takwimu sahihi ya idadi ya watu itakayowezesha Serikali kupanga mikakati thabiti kwa maendeleo ya Taifa.’Alisisitiza’

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa