• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC IBUGE AMESISITIZA KUTUMIA MFUMO WA GOTHOMIS KWENYE VITUO VYA AFYA IFIKAPO SEPT MOSI 2021.

Tarehe ya kuwekwa: June 11th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Generali Wilbert Ibuge ameongoza kikao kazi cha kufanya tathimini juu ya utoaji wa huduma bora za afya kwa Mkoa wa Ruvuma, kikao kilichofanyika  hapo jana  tarehe 10 Juni 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Kikao ambacho kilijumuisha wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma, Wakurugenzi wa Halmashauri 8, Wenyeviti wa Halmashauri Pamoja na viongozi mbalimbali, kwa lengo la kujenga uelewa juu ya utoaji huduma bora za afya kwa jamii.

Akizungumza wakati  wa ufunguzi wa kikao hicho Generali Ibuge amesema kwamba lengo kuu la kuitisha kikao cha pamoja na viongozi wote ni kuongeza uelewa na uwajibikaji katika kusimamia sekta ya afya hususani upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya afya pamoja na ukusanyaji wa mapato kwa njia ya mfumo wa GOTHOMIS.

Ibuge amemtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kupitia Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma  kuwasilisha taarifa ya kila robo mwaka kuhusiana na hali ilivyo katika utoaji wa huduma za afya kwa Mkoa wote wa Ruvuma pamoja na kuainisha changamoto mbalimbali ambazo zinajitokeza hasa katika Nyanja ya upatikanaji wa dawa na ukusanyaji wa mapato ili kuweza kukabiliana nazo na kuleta maendeleo katika sekta ya afya Mkoani Ruvuma.

Pia ametoa maagizo kwa viongozi hao,  ifikapo septemba mosi 2021 vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya umma katika Mkoa wa Ruvuma viwe vimefungwa mfumo wa kukusanya mapato kwa njia ya kidigitali GOTHOMIS,  na yeyote atakayeshindwa kutii agizo hilo hatua kali zitachukuliwa.“Ibuge alisisitiza”    

Ibuge aliongeza kuwa mapato na matumizi ya vyanzo vyote katika Halmashauri zote yawe yanajadiliwa kwenye vikao vya kisheria na kamati za ndani ya Halmashauri, na  kuhakikisha ukusanyaji wa mapato katika sekta afya ufikie asilimia 80% ili kuondoa changamoto ya ukosefu wa dawa katika vituo vya afya.

Aliongeza kuwa  kila Halmashauri ihakikisha wanahamasisha jamii kujiunga na mfuko wa huduma ya afya ya jamii ulioboreshwa iCHF ambapo mpaka sasa Mkoa Ruvuma umesajili kaya 18,039 ambayo ni sawa na asilimia 5% kati ya  kaya 12,203 ambayo ni  sawa na asilimia 3.4% zilizopo hai,  na  kaya 5,851 sawa na asilimia 1.6% ni kaya mfu.

Naye Mfamasia Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Shaloon Peter amesema hadi kufikia mwezi Mei 2021 Mkoa wa Ruvuma umepata jumla ya Tshs. 3,752,463,234.89 ambayo ni sawa na asilimia 80.1% kwa ajili ya ununuzi wa bidhaa za afya ambapo katika fedha hizo Mkoa umetumia Tshs. 1,530,397,382.84 ambayo ni sawa asilimia 40.78%.

 

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA;

11.06.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa