• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC IBUGE AZINDUA RASMI ANUANI ZA MAKAZI NA POSTI KODI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: February 15th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

15.02.2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Generali Balozi Wilbert Ibuge amezindua rasmi zoezi la uwekaji wa anuani za makazi huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa viongozi wanaosimamia zoezi hilo.

Ibuge amezindua mpango huo hapo jana Februari 14, 2022 katika eneo la NMB Bank lililopo Manispaa ya Songea ikiwa ni siku chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kutoa maagizo kwa wakuu wa Mikoa nchini kusimamia mpango huo kikamilifu.

Akizungumza kabla ya kuzindua mpango huo, Ibuge alisema kuwa mfumo wa anuani za makazi ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa na hivyo ni lazima kila kiongozi ajitoe katika kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa kwa muda maalumu uliopangwa na serikali.

Alisema utekelezaji wa mpango wa uwekaji wa anuani za makazi na posti kodi unagharamiwa na Serikali kwa shilingi bilion 28 ambapo  kwa mujibu wa maagizo ya Rais yaliyotolewa Februari 8, 2022 amewataka wakuu wote wa Mikoa kusimamia zoezi hilo ili ifikapo mwishoni mwa mwezi Mei 2022 liwe limekamilika, ikiwa  kwa Mkoa wa Ruvuma zoezi imeadhimiwa  kukamilika ifikapo  Aprili 31, 2022. “Alibainisha”

Amewataka wakuu wa Wilaya, wakurugenzi pamoja na viongozi wa ngazi zote kujipanga kikamilifu ikiwa ni pamoja na kushirikiana na wananchi katika kutekeleza zoezi hili bila kuwepo na malalamiko kutoka kwa wananchi.’Alisisitiza’

Ametoa rai kwa wananchi wote Mkoani Ruvuma kushiriki kikamilifu kuelekea zoezi la sensa ya watu na makazi inayotarajia kufanyika mwezi Agosti mwaka huu kwa lengo la kupata idadi kamili ya watu itakayosaidia katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwa wananchi.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Steven Ndaki alieleza kuwa chimbuko la uwekaji wa anuani za makazi ni utekelezaji wa sera ya Posta ya mwaka 2003, ambayo inazitaka nchi wanachama kuanzisha mfumo wa anuani za makazi na posti kodi kwa mujibu wa sheria za Serikali za mitaa; mamlaka ya mji sura ya 247 ambayo imetoa mamlaka ya kuzipa majina barabara na kutoa namba kwenye nyumba za wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema,  akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya Mkoani Ruvuma  alisema kuwa wamejipanga kusimamia na kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa ufanisi kwa kufuata miongozo na taratibu zilizotolewa na Serikali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema zoezi hilo kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea litafanyika katika kata 21, mitaa 95, barabara zilizo chini ya TARURA 403 pamoja na nyumba elfu 64,906 ambazo zimehesabiwa kwa mujibu wa taarifa ya awali iliyotolewa ambapo ameahidi kusimamia zoezi hilo kikamilifu na kwa wakati.

Uzinduzi huo ulihitimishwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kukabidhi kibao cha anuani ya makazi kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea pamoja na kuweka rasmi kibao kuonyesha jina la barabara iliyopo Manispaa ya Songea yenye jina NMB Bank Songea, 2 barabara ya NMB, 57101 Songea Ruvuma ikiwa ni kiashiria cha uzinduzi wa zoezi la uwekaji anuani za makazi na posti kodi.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa