• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC IBUGE KUTATUA CHANGAMOTO ZA ARDHI MKOANI RUVUMA.

Tarehe ya kuwekwa: July 14th, 2021

viongozi Mkoani Ruvuma wanatakiwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi  ya  kujikinga dhidi ya ugonjwa hatari wa CORONA ikiwemo na kuchukua tahadhari kwenye maeneo ya Mikusanyiko  mbalimbali kwa kuhakikisha  wananchi wanachukua tahadhari  kwa kunawa mikono kwa maji tiririka, kutumia vitakasa mikono, pamoja na kuvaa barakoa.

 Ibuge ametoa rai kwa wananchi Mkoani humo kufuata maelekezo yote yanayotolewa na wataalamu wa Afya ili kujikinga na wimbi la tatu la ugonjwa hatari wa CORONA ambapo alisema Mkoa wa Ruvuma bado haujawa tishio kwasasa,  bali amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwani kujikinga ni bora kabla  ya kuugua.

Hayo yamebainishwa katika  kikao kazi cha watumishi wa Sekta ya Ardhi Mkoa  wa Ruvuma kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea tarehe 13 julai 2021 ambapo mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, kilichohudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi kutoka Halmashauri 8, pamoja na maafisa Tawala Wilaya kwa lengo la kufanya tathimini ya utekelezaji wa kazi za ardhi kwa mwaka 2019 hadi 2020 na kuweka malengo  ya mwaka 2021/ 2022 pamoja na  mikakati ya  utatuaji wa  migogoro ya ardhi kwa wananchi.

                                                                                                                                              

Alisema,  azma kuu ya Serikali ni kuboresha utendaji kazi, kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa Sekta ya Ardhi nchini kwa kuondoa / kupunguza malalamiko  kwa wananchi ikiwemo na  kutoa huduma bora na kwa kuzingatia maadili ya kazi pamoja  na  Kutojihusisha na vitendo vya rushwa, sambamba na  kuwatembelea wananchi katika maeneo yao badala ya kusubiri migogoro hiyo iwakute Ofisini.

Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa Sheria ya Mipangomiji Namba 8 ya Mwaka 2007 Fungu la 7 kifungu kidogo cha (1),  Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya ni Mamlaka za Upangaji (Planning Authorities), na  kifungu kidogo cha (5) cha Sheria ambayo inaelekeza mambo muhimu yanayopaswa kufanywa na Mamlaka za Upangaji.

Ametoa  wito kwa viongozi hao  kuweka utaratibu wa kufanya vikao vya wataalamu wa ardhi mara kwa mara ili kubaini changamoto mbalimbali za wananchi na kuweka mpango mkakati wa  utatuzi wa changamoto hizo. “Brigedia Ibuge alisisitiza”

 

Naye kamishna wa Ardhi Mkoa wa Ruvuma Ildefonce L. Ndemela alisema katika mwaka wa fedha 2020/2021, Ofisi ya ardhi Mkoa wa Ruvuma imesimamia na kutekeleza kazi za upangaji, upimaji, umilikishwaji, uthamini, usajili wa Hati na nyaraka mbalimbali, utatuzi wa migogoro ya Ardhi na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali ambapo kwa mwaka wa  Fedha 2020 / 2021, Mkoa wa Ruvuma ulipangiwa malengo ya kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni  4.6  ambayo walikusanya  kwa asilimia 87%, pia kwa  mwaka wa fedha 2021/2022 Mkoa umepangiwa malengo ya kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 3.0.

Ndemela alibainisha baadhi ya changamoto mkoani Ruvuma ni pamoja na Upungufu wa Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya katika baadhi ya Mabaraza yaliyopo Mkoa wa Ruvuma, Upungufu wa vitendea kazi kama printer, plotter na mashine ya kudurufu kwa baadhi ya Halmashauri kwa ajili ya kutengeneza Ankara za malipo pamoja, ilani za madai ya kodi pamoja na nyaraka zingine.

Katika kutatua changamoto hizo Mkoa wa Ruvuma umeweka mikakati ambayo ni pamoja na kuajiri watumishi wa kada ya ardhi, Kuhakikisha  wadaiwa sugu wote wanapelekewa notisi za madai ya kodi  na kuwafikisha mahakamani kwa wale ambao watakaidi kulipa kodi kwa wakati, Kufanya matangazo mbalimbali kwenye vyombo vya habari, kufanya matangazo ya kuzunguka mtaa kwa mtaa na kubandika vipeperushi vya kuwakumbusha wamiliki kulipa kodi ya pango la Ardhi, Kushirikiana na Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa kusambaza ilani za madai ya kodi ya pango la Ardhi, Kushirikiana na Mamlaka za upangaji katika zoezi la upimaji pamoja na urasimishaji wa makazi holela, kwa ajili ya kuongeza viwanja vipya ili kuongeza milki mpya na makusanyo. “Ndemela Alibainisha”

 

  • NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI- SONGEA MANISPAA;

14 julai 2021. 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa