• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC MNDEME AMEWATAKA VIONGOZI WA TAASIS KUTATUA KERO ZA WANANCHI.

Tarehe ya kuwekwa: April 14th, 2021

                                    

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewataka wakuu wa Taasisi na Idara mbalimbali Mkoani Ruvuma kuweka utaratibu wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa lengo la kupunguza migogoro inayowakabili wananchi.

Hayo yametolewa katika kikao cha wakuu wa Taasisi na Idara mbalimbali Mkoani Ruvuma kwa lengo la utatuzi wa kero kwa wananchi kilichofanyika leo tarehe 14 aprili 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mndeme alisema kila Kiongozi anatakiwa atimize wajibu wake  wa kazi aliyopewa pamoja na utatuzi wa kero mbalimbali za wananchi ikiwemo na kero ya Maji, Umeme, Barabara, Miundombinu ya shule na Ardhi. Aliongeza kuwa  endapo viongozi  wataendelea kufanya kazi maofisini bila kwenda kwa wananchi kuibua  kero zinazowakabili wananchi hao  kutapelekea uwepo wa malalamiko mengi ambayo itapelekea kuyapeleka ngazi ya juu (Mkoani).

Aliongeza kuwa uwepo wa kero nyingi za wananchi huashiria  kutojituma kwa viongozi waliopo katika nafasi zao za kazi ambapo viongozi hao wanapaswa kutimiza wajibu wao wa kazi sambamba na kutatua kero za wananchi bila kusubiri viongozi wa Kitaifa watatue kero hizo.

Amewaagiza Wakuu wa Taasisi na Idara kuunda mkakati maalumu wa kutatua kero za wananchi kuanzia ngazi ya chini kwa kuweka utaratibu wakuratibu kero hizo kwenye rejista ambazo  zitaonyesha aina ya kero, Idara husika na namna gani imetatuliwa na endapo itakua haijatatuliwa ipelekwe ngazi ya juu (Mkoa) kwa utatuzi Zaidi.

Alisema “Ukosefu wa mahusiano mazuri miongoni mwa viongozi, kutofanyika vikao vya kisheria na kutokuwa na matumizi mazuri ya Lugha kwa wananchi hupelekea kutokea kwa malalamiko/kero kwa wananchi”.

Amewaagiza Viongozi hao kuhakikisha kila ifikapo mwishoni mwa mwezi kufanya tathimini ya utekelezaji wa zoezi hilo la utatuzi wa kero kwenye Taasisi yake, uwasilishaji  wa taarifa ya kero zinazohitaji utatuzi wa kisera, uandaaji wa  rejista ya malalamiko ya wananchi, uundaji  wa  timu ndogo ya kuratibu na kutatua kero za wananchi pamoja na kikao cha tathimini cha majumuisho ya utekelezaji wa zoezi la utatuzi wa  kero kila ifikapo robo ya  mwaka. “Mndeme alibainisha”.

Mndeme amewataka wafanyabiashara Mkoani Ruvuma kuuza bidhaa/vyakula kwa bei rafiki  katika kipindi hiki cha mfungo wa Ramadhani ili bidhaa za chakula zipatikane kwa urahisi kwa Waislamu wanaoshiriki kwenye mfungo wa Ramadhani.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho amewataka wataalamu kutekeleza wajibu wao ikiwemo utekelezaji wa agizo lililotolewa katika kikao cha RUWASA ambalo lilikuwa linahusu utatuzi wa kero ya maji kwa wananchi.

Oddo alisema kila mtaalamu anatakiwa kujituma katika nafasi yake ya kazi ili wananchi waweze kupata huduma thabiti inayotolewa na Serikali yao.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

14/04/2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa