• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC RUVUMA , Akasirishwa na tabia ya Migomo, Matusi na Kashifa hazina tija kwa karne ya leo. HAPA KAZI TU.

Tarehe ya kuwekwa: March 10th, 2021

UONGOZI ni kazi, uongozi unahitaji uwezo wa mungu, uongozi unahitaji hekima, kiongozi hutoka kwa mungu, uongozi sio mvutano bali ni kukaa mezani kwa pamoja na kusikilizana,  nawaombeni tutumie hekima na busara njia  sahihi ya kuwasilisha hoja zenu ni vikao sio mgomo na kutumia lugha chafu.

Mungu wetu wa mbinguni akatawale mawazo yetu na hekima yetu,  nitawapenda na kuwajali kila siku  . ” nimewasamehe kutoka moyoni mwangu”

Kauli hiyo imetamkwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme katika kikao na wafanyabiashara Mkoa wa Ruvuma kilichofanyika 09 machi 2021 katika  ukumbi wa Parokia ya Mtakatifu Bombambili kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero za wafanyabiashara Mkoani Ruvuma.

Mndeme alisema wafanyabiashara mnatakiwa kuwa wakweli wakati wa utoaji wa taarifa  hakikisheni taarifa zenu zinakuwa  sahihi,  zenye takwimu sahihi, na unapoongea na kiongozi kama MH. Rais unatakiwa kujipanga usikurupuke sababu MH. Rais ni kiongozi mkubwa wa Nchi.

Aliongeza kuwa baadhi yao wafanyabiashara wametumia fedha nyingi sana kuhakikisha stendi inarudi Mfaranyaki, na  kulishana sumu na kuhamasisha mgomo na hatimaye wengine wakafunga maduka yao na wengine wakapiga simu na kujisafisha kuwa hawapo kwenye mgomo, huo ni unafiki ‘ acheni unafiki’ na unafiki ni mbaya sana. ‘” Kama mnaamua kufunga maduka fungeni na kama mnaamua kufungua maduka fungueni.  Hakuna nguvu ya pesa  bali njia ya kutatuwa mgogoro ni vikao sio nguvu ya pesa. “ Mndeme alisema”

Serikali haiendeshwi kwa vitisho bali Serikali hii inaendeshwa kwa mujibu wa katiba na sheria sio mihemuko na matusi. Mkikubaliana jambo kubalianeni sio mnakuwa wanafiki. “ alikemea”

Alisema tangu awepo kiongozi huyo katika Mkoa wa Ruvuma hajawahi kuona wafanyabiashara wa Mkoa wa Ruvuma wanamshukuru MH.Rais kwa kazi nzuri alizozifanya tangu aingie madarakani badala yake mnatengeneza migogoro ambayo haina msingi.

Aliongeza kuwa tangu nchi hii ipate uhuru Mkoa wa Ruvuma haujawahi kupata umeme wa (grid) ya Taifa wenye thamani ya Bilioni 216, lakini kipindi umeme unasumbua militia viongozi  ili waweze kutatua tatizo hilo.

Akiyataja mafanikio yaliyofanyika Mkoani Ruvuma chini ya uongozi wa Serikali ya awamu ya tano ambayo wafanyabiashara Mkoani humo hawajawahi kumshuru mh. Rais ni pamoja na matengenezo ya barabara yenye kiwango bora cha Lami kutoka Tunduru hadi Songea ambapo hapo  awali wafanyabiashara hao  walipata adha ya kusafirisha bidhaa zao kwa kutumia magari aina ya WANTEN ambapo kwasasa changamoto hiyo imekwisha.

Aliongeza kuwa wafanyabiashara hawajawahi kutoa tamko la kumshukuru MH.Rais kuwezesha upatikanaji wa huduma ya maji safi ndani ya Manispaa ya Songea, ujenzi wa uwanja wa ndege Songea, ongezeko la  meri tatu za mzigo Nyasa, pamoja na ongezeko la vituo vya afya. alisema “ inahitaji  ujasili kuongea na watu waliokutukana, ila nimewasamehe. Migomo, matusi na kashifa havina tija kwa karne ya leo. HAPA KAZI TU.” 

Aliwapongeza wafanyabiashara ambao hawakufunga maduka na kuruhusu mabasi yao kusafirisha abiria, na kwa wale ambao waligoma kusafirisha abiria kutoka Songea mjini kwenda Mbinga Mjini walifutiwa leseni zao na kuwaruhusu LATRA kupokea usajili kwa wanaohitaji kusafirisha abiria kupitia njia hiyo na  endapo itatokea kugoma tena  kusafirisha abiria zitafutwa leseni zao kwasababu lessen  ni mali ya Serikali.

Alisema kabla stendi ya Tanga kuanza kazi Manispaa ya Songea ilikuwa inakusanya Tsh 150,000/= kwa siku lakini baada ya kuanzishwa kwa stendi ya Tanga Manispaa ya Songea inakusanya Tsh 900,000 hadi milioni moja 1,000,000/=.

Lengo kuu ni kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa daladala waweze kupakia na kushusha abiria kutoka Tanga kuelekea mjini na kuondoa mtazamo wa upande mmoja tu ikiwaa wadaldala nao wanahitaji kupata huduma hiyo. Alisema tumezuwia kushusha abiria stendi ya Mfaranyaki ili stendi ya Tanga iweze kufanya kazi. Stendi itakayo bakia kupakia abiria ni stendi ya Seedfarm na Ruhuwiko tu.

Alibainisha baadhi ya Mikakati ya Halmashauri ya Manispaa  ya Songea ya kuboresha huduma za stendi ya Ruhuwiko  ni pamoja na kujenga uzio kuzunguka eneo  la  shule ya Ruhuwiko, kujenga vivuli vya kujikinga na mvua kwa abiria, na kuboresha stendi ya Ruhuwiko pamoja na kuongeza idadi ya matundu ya vyoo.

Naye mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho alisema ‘”acheni mgogoro, endapo mkiendeleza mgogoro tutaiharibu  Ruvuma yetu. Tunachotakiwa kufanya ni  kujenga umoja wetu  na lazima tuangalie  kila maeneo yana tamaduni zake na desturi zake za kitanzania ambazo tunatakiwa tuzifuate, na mgomo huo ni shinikizo la baadhi ya viongozi na wengine huogopa sababu ya nguvu za giza”.

Oddo alisema Mkurugenzi wa Manispaa Tina Sekambo ameteuliwa na MH. Rais na kutokana na utendaji wake bora wa kazi ataendelea kubaki Manispaa ya Songea.

Amewataka Madiwani hao  kuacha tabia ya kuchochea ugomvi ambapo baadhi yao hujificha ili wasifahamike na huku wakiendelea kuchochea ugomvi lakini  baada ya kubaini hilo aliwaita viongozi hao na kuwaonya. “Madiwani kama hao ni dhaifu” Alisisitiza.

Naye katibu mkuu jumuiya ya wafanyabiashara Taifa Abdalah Mwinyi alitoa wito kwa wafanyabiashra hao kujihepusha na siasa, ambapo alisema mkitaka kuharibu mwenendo wa Taasis jihusisheni  na siasa japo maisha yetu ni siasa.

Mwinyi aliomba radhi kwa viongozi  kwaniaba ya wafanyabiashara hao kwa lugha chafu zilizotolewa wakati wa mgomo wa wafanyabiashara hao. 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

10.03.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa