• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RUWASA " MAJI BOMBANI, PESA BENK"

Tarehe ya kuwekwa: January 29th, 2021

Fedha zote zitokanazo na mauzo ya maji zikaguliwe na Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri husika ili kujiridhisha na matumizi ya fedha za wananchi.

Agizo hilo  limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  katika kikao cha wadau wa maji Mkoa wa Ruvuma RUWASA kilichofanyika leo 29 januari 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mndeme alisema kikao hicho kinalenga kuzungumzia kiundani majukumu ya kazi  mbalimbali za Serikali za mitaa, Sekta binafsi, huduma za maji na usafi wa mazingira vijijini chini ya usimamizi wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma,  mafanikio, na changamoto za utekelezaji wa Sekta ya Maji mijini na vijijini tangu kuanzishwa kwa wakala wa maji na Usafi wa mazingira “RUWASA”.

 Alisema mnamo tarehe 01 julai 2019 Serikali iliandaaa na kushusha sheria ya maji namba 5 ya mwaka 2019 ambayo inaongoza mambo yote  tunayohitaji kutekeleza katika masuala ya huduma za maji vijijini na mijini katika adhima ya kuwavutia wananchi maji vijijini.

Sera ya maji ya 2002 na sheria namba 5  ya mwaka 2019 inasisitiza Miradi ya maji iendeshwe na wananchi wenyewe na kuchangia sehemu  za gharama za ujenzi  na gharama zote za uendeshaji na usimamizi wa rasilimali za maji.

Amewataka mameneja wa Wilaya RUWASA na Halmashuri za Wilaya  kufanya kazi kwa bidii katika kuhamasisha uundaji wa vyombo vya watumiaji  maji  ukilinganisha na takwimu zilizotolewa za  vyombo vya watumiaji maji vilivyosajiliwa ni 79.

Kwa kutokana na takwimu hizo zilizotelewa ameagiza kila Wilaya ijipange na ihakikishe inasimamia na kuunda vyombo vya watumiaji maji ili kuleta tija na ufanisi mkubwa na kuwa endelevu.

Aliwapongeza wadau wa  maji wakiwemo wananchi kwa kujenga miradi ya maji kwa kujitegemea wenyewe pamoja na kamati ya siasa CCM Mkoa na Wilaya kwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa sekta ya maji na kuleta msukumo mkubwa ili miradi iweze kuendelea Zaidi.

Mndeme ametoa pongezi kwa Serikali ya awamu ya tano iliyoongozwa na Mheshimiwa Dr. John Pombe Magufuli  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  kupitia Wizara ya maji kutoa fedha za kutosha Mkoa wa Ruvuma za ujenzi wa miradi ya maji pia na maamuzi mazuri ya kubadili mfumo wa miradi kwa kutumia force account badala ya kutumia wakandarasi.

Alisema ili miradi iweze kuwa endelevu yafuatayo ni muhimu “ Halmashauri na sekritariet ya mkoa kuwajibika kikamilifu katika kutekeleza na kusimamia majukumu yote yaliyoorodheshwa katika sheria namba 5 ya huduma za maji za 2019, Mameneja wa RUWASA kutoka Wilaya zote za mkoa wa Ruvuma kushirikiana na Halmashuri zote kuhakikisha miradi iliyopo na mingine itakayojengwa inaundwa na vyombo huru vya watumiaji maji kabla au ifikapo 31 mei 2021.”

Maafisa Tarafa, viongozi wote ngazi ya Wilaya kwa kushirikiana na  Wakuu wa Wilaya kusimamia  kusimamia utunzaji wa vyanzo vya maji   na kuhakikisha kikao cha baraza la madiwani cha kila robo kuwepo kwa mada ya kudumu ambapo Meneja wa RUWASA wa Wilaya  husika watatakiwa kutoa hali ya uundaaji na usajili vyombo vya watumiaji maji. Mndeme alisisitiza.

Alisema ni marufuku kwa mtu yeyote atakaye haribu miundombinu ya vyanzo vya  maji wakibainika wachukuliwe hatua za kisheria.

Naye mwenyekiti wa CCM mkoa  wa Ruvuma  Oddo Mwisho alishauri kuwa kutokana na muungozo huo kila Halmashauri za Wilaya kila wanapokaa kupanga bajeti ni lazima washirikishe wataalamu wa maji Ruwasa ili kuweza kuweka vipaumbele vya Halmashauri husika kupitia changamoto inayowakabili wananchi wa Mkoa wa Ruvuma.

Kauli mbiu iliyotolewa. Magufuli- Maji bombani

                                           RUWASA- “ Maji bombani, pesa Benk”

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

29.01.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa