• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SACCOS MANISPAA YA SONGEA YAENDELEA KUTOA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU.

Tarehe ya kuwekwa: December 11th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

11.12.2021

Chama cha ushirika cha akiba na mikopo (SACCOS) Manispaa ya Songea chajipanga kutoa mafunzo kwa wanachama, watendaji na viongozi kwa lengo la kuongeza uelewa na ufanisi wa kazi katika chama hicho.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa SACCOS Manispaa ya Songea Amiry Ayoub katika mkutano wa 29 wa mwaka huu leo tarehe 11 Disemba 2021 uliofanyika katika ukumbi wa AJUCO Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, pamoja na wanachama wa chama hicho.

Amiri alieleza kuwa kwa mwaka 2021 chama hicho kimefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni 613, 522, 000 kutoka kwenye makusanyo ya ndani ambapo katika fedha hiyo shilingi milioni 396, 850, 00 imetumika kutoa mikopo kwa wanachama 169.

Alisema kuwa miongoni mwa changamoto zinazokikabili chama hicho ni pamoja na baadhi ya wanachama kushindwa kurejesha mikopo yao kwa wakati, wanachama wanaochangia akiba kwa fedha taslimu kushindwa kuchangia kwa wakati pamoja na baadhi ya wananchama kuuza mikopo yao kwa Taasisi kubwa za kifedha hali inayopelekea chama kukosa mapato.’Alibainisha’

Aliongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2022 chama kimejipanga kuongeza msukumo wa ukusanyaji wa hisa, akiba na hisa za hiari kwa lengo la kukuza mtaji wa chama kwa kubuni vyanzo mbalimbali vya mapato ya chama hicho, kutoa huduma bora kwa wanachama kwa wakati kulingana na mwongozo pamoja na kuongeza wigo wa huduma ili kupata wananchama wengi Zaidi.

Kwa upande wake Meneja wa SACCOS Manispaa ya Songea Winifrida Komba alisema kuwa chama hicho kilianzishwa kwa lengo la kuwanufaisha kiuchumi wafanyakazi wote wa umma waliopo ndani ya Manispaa ya Songea ambapo hadi sasa chama hicho kimefanikiwa kujiendesha chenyewe kwa kupitia fedha zinazokusanywa kwa mapato yake ya ndani.

Naye Afisa ushirika Manispaa ya Songea Given Mariki ametoa rai kwa wanachama wote waliokopa fedha na kushindwa kurudisha kwa wakati kuhakikisha wanarudisha fedha hizo kabla ya hatua kali za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Ametoa pongezi kwa bodi ya uongozi wa chama hicho kwa kufanikiwa kuongeza wanachama wapya 14 kwa mwaka 2021 na amewataka wafanyakazi ambao bado hawajajiunga na chama hicho kuchukua hatua kwa kujisajili ili kuweza kujiinua kiuchumi.

Wakizungumza kwa wakati tofauti wanachama wa chama hicho wamesema kuwa miongoni mwa faida ya kujiunga na SACCOS Manispaa ya Songea ni pamoja na kupata  mkopo wa riba nafuu ambayo huwasaidia wanachama  kutatua changamoto mbalimbali pamoja na kuipongeza  bodi ya uongozi kwa usimamizi mzuri wa mapato ya chama na uwepo wa mikakati thabiti ya chama iliyowekwa.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa