• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAPINGA UNYANYASAJI WA WANYONGE.

Tarehe ya kuwekwa: August 11th, 2020

Kauli hiyo imetolewa na  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi Mh. William Lukuvi katika uzinduzi wa Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Ruvuma na mpango kabambe wa Manispaa ya Songea iliyofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma tarehe 10/08/2020.

Lukuvi alisema lengo la  Serikali  kuhakikisha kwamba inatoa huduma stahiki kwa wananchi wote wa Mkoa Ruvuma kwa halmashuri zote 8 (nane) ili kuwapunguzia  wananchi usumbufu wa kufuata huduma  mbali pamoja na  kuwarahisishia wananchi kwa kujipatia maendeleo yao kwa kutumia ardhi waliyonayo.

Awali Wizara ilianzisha ofisi za kanda tano ambazo zilikuwa zikisimamiwa na Kamishina wa Ardhi wasaidizi, baadae kanda hizo ziliongezeka kutoka tano hadi tisa (9) mwaka 2019 ambapo Mkoa wa Ruvuma ulikuwa ukihudumiwana Kanda ya kusini iliyokuwa na ofisi katika Mkoa wa Mtwara.

 Aidha, alisema pamoja na uwepo wa Ofisi hizo tisa za Kanda bado wananchi walikuwa wakipata usumbufu wa kutumia gharama kubwa za usafiri ili kupata huduma za ardhi ikiwemo na hatimiliki na nyaraka mbalimbali, ili kuondoa adha hiyo mwezi marchi 2020, Wizara imeanzisha ofisi za Ardhi za Mikoa katika Mikoa yote 26 Nchini.

Alibainisha kuwa Mkoa wa Ruvuma una vijiji 144 ambavyo havijapimwa  kati ya Vijiji 544, kati ya hivyo vilivyopimwa vijiji 300 havijapewa hati ya ardhi, hivyo aliwaagiza Wataalamu hao ndani ya miezi mitatu Vijiji vyote viwe  vimepewa hati ya kutambulika kama kijiji ili kupata mipaka ya kiutawala kwa kila kijiji na kuondoa migogoro baina ya kijiji na kijiji jirani.

Hata hivyo aliwaagiza Wakurugenzi wote kusimamia na kupanga matumizi bora ya ardhi kwa kila kijiji ili mji uweze kupanga vizuri na itasaidia wananchi kupanga matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya ujenzi wa majengo ya taasisi, makazi, mashamba pamoja na  matumizi mengineyo ya ardhi.

Alisema uwajibikaji na uadilifu kwa wataalamu katika kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo  pamoja na ukusanyaji wa mapato yanayotokana na  kodi za ardhi mkoani Ruvuma pamoja na kufanya kazi kwa kufuata miongozo  na kanuni katika kuhakikisha ulipaji wa fidia za ardhi, uchoraji, na uizinishaji wa hati miliki unatekelezwa iapasavyo. Alisisitiza.

Aliongeza kuwa hakuna sababu ya kuchukua ardhi kwa uonevu bila kulipa fidia bali kila mtu mwenye haki ya kulipwa fidia nilazima alipwe fidia yake., Alitoa agizo kwa kila Halmashauri zote lazima ziweke sanduku la maoni pamoja na daftari la  malalamiko ili kupokea kero kwa wananchi na zionyeshe namna gani kero hizo zimetatuliwa.

Baada ya hotuba hiyo, alifungua ofisi ya ardhi Mkoa wa Ruvuma na kuzindua Mpango kabambe wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea pamoja na kugawa hatimiliki 27 kwa wananchi wa Manispaa ya Songea.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY, 

KAIMU AFISA HABARI- MANISPAA YA SONGEA.

11/08/2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa