• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI YATOA MASAA 24 KWA WAFANYABIASHARA KUFUNGUA BIASHARA ZAO.

Tarehe ya kuwekwa: February 22nd, 2021

 

Serikali itaendelea kusimamia matumizi sahihi ya stendi ya Mfaranyaki kama ilivyoamriwa kupitia vikao vya kisheria vya Baraza la Madiwani la Manispaa ya Songea, kwa ajili ya matumizi ya usafiri wa daladala na sio vinginevyo.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Songea Cosmas M. I. Nshenye katika kikao na Waandishi wa Habari kwa ajili ya kutoa tamko kwa wafanyabiashara wote na wenye vyombo  vya usafirishaji kurudisha huduma zao ndani ya masaa 24 kilichofanyika  leo 22 februari 2021  katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Songea.

Nshenye amesema ukiwa  mfanyabiashara  tayari utakuwa umeingia kwenye mkataba na Serikali pia mfanyabiashara yeyote anatakiwa kufahamu athari za mgomo zitakazotokea na wanaoathirika sio Serikali pekee bali kuna athari za kijamii, kiuchumi na nyinginezo.

Ameagiza Afisa wa  LATRA “kufuta mara moja route ya mabasi yote yanayotoa huduma ya usafirishaji kuanzia Songea mjini hadi Mbinga Mjini na  kwa mfanyabiashara yeyote mwenye nia ya kutoa huduma za usafirishaji abiria kutoka Songea Mjini  hadi Mbinga Mjini aombe mara moja ili aweze kufanya shughuli za usafirishaji katika route hizo”. Pia Serikali itaendelea kufuatilia mwenendo wa route nyingine ili kuona ufanisi wake katika kuhudumia  wananchi. Nshenye amesisitiza.

Alisema Serikali ina taarifa kupitia vikao vilivyofanyika hivi karibuni vya wafanyabiashara kuwepo kwa matamshi ya lugha za matusi, uchochezi na uvunjifu wa Amani na kuhujumu mipango ya Serikali katika kutoa huduma kwa wananchi.

Amewataka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi mara moja na kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wahusika wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo, pamoja na kuweka Mpango mbadala wa haraka wa utatuzi wa suala la usafiri katika kurudisha huduma za usafiri.

Ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea na LATRA kuwachukulia hatua za kisheria kwa mujibu wa Sheria za Leseni ikiwepo kuwanyang’anya Lesen za biashara wahusika wote watakaokaidi maelekezo ya kurudi kazini/ kufungua biashara zao ndani ya masaa 24 toka tamko hili limetolewa.

Mwisho aliwashukuru wananchi na wadau wote kwa utulivu mkubwa katika kipindi hiki ambacho Serikali  imeendelea kushughulikia changamoto pamoja na wadau  walioendelea kutoa huduma na kupuuza matamko yaliyotolewa na watu wasiokuwa na nia njema na Serikali yao.

 IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

22.02.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa