• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SHAKA ATOA MAAGIZO KUHUSU UNUNUZI WA MAHINDI SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: September 21st, 2021

Katibu wa Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa itikadi na uenezi Shaka Hamdu Shaka amewataka wakala wa chakula Mkoa wa Ruvuma (NFRA) kuweka utaratibu mzuri ili kumaliza utata uliopo juu ya zoezi la ununuzi wa mahindi Manispaa ya Songea.

Hayo yalibainishwa wakati alipotembelea kituo cha wakala wa chakula Taifa (NFRA) kilichopo ndani ya Manispaa ya Songea hapo jana tarehe 20 Septemba 2021 wakati akihitimisha ziara yake ya  siku mbili  Mkoani  Ruvuma kwa lengo la kukagua  miradi ya Maendeleo ambayo ni utekelezaji wa ILANI ya CCM.

Shaka alisema kuwa wakala wa chakula (NFRA) ahakikishe  wananchi wote ambao wameorodheshwa idadi ya mahindi yao, yananunuliwa kwa wakati pamoja na kuongezwa kwa kituo kingine cha ununuzi wa mahindi  ili kupunguza msongamano katika kituo kinachotumika sasa na kuondoa usumbufu kwa wananchi.’Alisisitiza’

Aliongeza kuwa  Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 50 kwa ajili ya ununuzi wa mahindi na amewaahidi wakulima Tani thelathini na tano elfu za mahindi zitanunuliwa mwaka huu katika Mkoa wa Ruvuma pamoja na kutafuta masoko  nje ya Nchi. 

Pia alitembelea mradi wa ujenzi wa bwalo la sekondari ya Emmanuel Nchimbi ambapo aliahidi kutoa kiasi cha shilingi milioni 30 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa mradi huo sambasamba na Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt. Damas Ndumbaro naye aliahidi kutoa shilingi milioni 20 kwa lengo la kukamilisha kiasi kilichobakia kumaliza ujenzi wa bwalo hilo ambacho kilikuwa ni shilingi milioni 50.

Shaka alihitimisha ziara yake katika Mkoa wa Ruvuma kwa kutembelea mradi wa ujenzi wa madarasa 2, ofisi 1 na ukamilishaji wa madarasa 3 katika shule ya msingi Amani iliyopo kata ya Mjimwema Manispaa ya Songea pamoja na mradi wa ujenzi wa boksi kalavati na barabara ya BP station-Sangawani ya KM 1.1 kwa kiwango cha lami nyepesi  na kuridhishwa na ukamilishwaji wa miradi hiyo.

IMETOLEWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

21.09.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa