• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini yawahimiza Watumishi kujiunga na vyama vya Wafanyakazi

Tarehe ya kuwekwa: November 12th, 2024

Katibu tawala Msaidizi wa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Damas Dominic Suta, amewataka watumishi katika mkoa huo kujiunga na vyama vya wafanyakazi, akisisitiza kuwa sheria ya ajira na mahusiano kazini inawataka watumishi ambao si wanachama wa vyama vya wafanyakazi kulipa ada ya uwakala ambapo  Hii ni kutokana na ukweli kwamba vyama vya wafanyakazi vinapodai haki za watumishi, hata wale wasiokuwa wanachama, wanapata faida ya huduma hizo.

Dkt. Suta alisema kuwa chama cha wafanyakazi kinaweza kupata hati ya usajili lakini kisitambulike rasmi na Serikali, na ili chama hicho kitambulike na Serikali, kinahitaji kuwa na usajili halali na kuwa na wanachama wengi zaidi kuliko vyama vingine, pamoja na kuhakikisha kinawakilisha maslahi ya wanachama, hata wale wasio wanachama.

Aidha,  alitoa wito kwa viongozi wa vyama vya wafanyakazi kusimama imara katika kusikiliza na kutatua changamoto za watumishi ambapo  Alisisitiza kuwa mara tu wanapopokea changamoto zinazohusu masuala ya utumishi, viongozi wanapaswa kufika kwa viongozi wa ngazi za juu ili kupata ufafanuzi na kutatua matatizo hayo kwa haraka.

Katika hatua nyingine, Dkt. Suta alitoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Idara za Ardhi kuhakikisha wanatenga bajeti ya kutosha inayotokana na mapato ya ndani ili huduma zinazotolewa na idara hiyo ziweze kufanywa kwa ufanisi na kwa viwango vinavyostahili.

Hayo yalisemwa na Dkt. Suta katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) Mkoa wa Ruvuma kilichofanyika tarehe 12 Novemba 2024 katika ukumbi wa Hazina Ndogo, Manispaa ya Songea ambapo Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe wa kamati ya utendaji wa TALGWU Mkoa wa Ruvuma.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TALGWU Mkoa wa Ruvuma, Wiley Luambano, alieleza kuwa mkoa wa Ruvuma unajivunia kuwa na wanachama 4,500 wa TALGWU wasiokuwa walimu huku akisisitiza kuhusu madai mbalimbali ya watumishi yasiyohusiana na mishahara, ikiwemo masuala ya uhamisho na likizo.

 Mwenyekiti Luambano pia alitoa shukrani kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuajiri watumishi 315 katika sekta ya afya, ambao tayari wameanza kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi.

IMEANDALIWA NA:
Amina Pilly
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa