• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SHERIA ya kumlinda mtoto isaidie kuzuia ajira kwa watoto

Tarehe ya kuwekwa: July 16th, 2018

UTUMIKISHAJI watoto wadogo bado unaendelea nchini, licha ya serikali kuweka sheria ya kumlinda mtoto mwenye umri usiozidi miaka 18.Nimepita katika baadhi ya maeneo mjini Songea na kubaini watoto wenye umri kati ya miaka tisa na 12 ambao wanazunguka kuuza bidhaa ndogo ndogo na wengine wanaombaomba.

Said Ally ni mtoto anayesoma darasa la pili katika shule moja katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambaye anafanya biashara ya kuuza karanga za kukaanga.“Nimeanza biashara hii tangu darasa la kwanza  nikitoka shuleni saa tano nafika mjini kuuza karanga katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya klabu za pombe,hadi kufika saa tisa nakuwa nimemaliza kuuza karanga ambapo kwa siku Napata sh. 5000’’,anasema.

Anadai pesa anayopata inamsaidia yeye na mama na wadogo zake kuendesha maisha kila siku,ingawa amekiri kuwa inamwathiri katika masomo yake kwa kuwa hapati muda wa kutosha kushiriki katika masomo.Uchunguzi ambao nimeufanya katika viunga vya mji wa Songea majira ya usiku kuanzia saa mbili hadi saa tano usiku nimeshuhudia watoto wadogo wakifanyabiashara hatarishi kutokana na mazingira.

Tatizo la kuwatumikisha watoto wadogo kazi halifanyiki  kwa ajili ya biashara pekee  bali pia watoto wameonekana  wakifanyishwa kazi katika maeneo mengine kama vile maeneo ya machimbo,kazi za ndani na uvuvi,kuponda kokoto na kufanyishwa vibarua.

Sheria ya haki za mtoto ya mwaka 2009, inabainisha wazi kuwa mtu hataruhusiwa kumuajiri au kumshughulisha mtoto katika aina yoyote ya kazi itakayomnyonya mtoto.Kwa mujibu wa sheria hiyo,mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya kutengwa au matendo yoyote yanayoweza kuwa na athari mbaya kwake kwa kuzingatia umri na uwezo wake.Tanzania ni miongoni mwa nchi 174 zilizoridhia Azimio la Umoja wa Mataifa namba 182 la kukomesha utumikishaji watoto chini ya umri wa miaka 18.

Makala haya yameandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Julai 16,2018



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa