• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SHERIA zinazokataza matumizi ya mifuko ya plastiki Tanzania

Tarehe ya kuwekwa: May 23rd, 2019

Kimsingi kuna *Makosa Makuu Matano* yaliyotajwa na kukatazwa ndani ya Sheria husika. Sheria hiyo Ndogo inajulikana kama *The Environmental Management (Prohibition of Plastic Carrier Bags) Regulations, 2019*. Sheria hii Ndogo imetungwa kwa Mujibu wa Kifungu Na. 230 (2) (f) cha Sheria inayojihusisha na Usimamizi wa Mazingira *(The Environmental Management Act, Cap. 191)*.


*A: MAKOSA*

Kwa mujibu wa Kifungu/Kanuni Na. 8 Cha Sheria ya Kuzuia Matumizi ya Mifuko ya Plastiki ambayo ni *The Environmental Management (Prohibition of Plastic Carrier Bags) Regulations, 2019* kuna Makosa Matano ambayo ni;

(A). Kuzalisha na Kuagiza Mifuko ya Plastiki,  *(Kifungu/Kanuni Na. 8 a )*;

(B). Kusafirisha nje ya nchi Mifuko ya Plastiki,  *(Kifungu/Kanuni Na. 8 b )*;

(C). Kuhifadhi na Kusambaza Mifuko ya Plastiki, *(Kifungu/Kanuni Na. 8 c )*;

(D). Kuuza Mifuko ya Plastiki, *(Kifungu/Kanuni Na. 8 d )*;

(E). Kumiliki na Kutumia Mifuko ya Plastiki? *(Kifungu/Kanuni Na. 8 e )*.


*B: ADHABU*

Kwa kila kosa tajwa hapo juu, Sheria husika imetaja Adhabu yake. Hivyo basi kuna Adhabu aina tano kama ilivyo kwa Makosa husika. Kifungu/Kanuni Na. 8 cha Sheria tajwa hapo kilichotaja Makosa Matano ndicho hicho kimetaja Adhabu ya kila Kosa kama ifuatavyo;


(A). *Adhabu kwa Wazalishaji na Waagizaji.*

Kifungu/Kanuni Na. 8 (a) cha Sheria tajwa hapo juu, kinataja Adhabu kwa Mtu au Watu hao kama ifuatavyo;

i. Faini isiyopungua *Milioni 20 na isiyozidi Billioni 1*,

ii. Kifungo Kisichozidi *Miaka Miwili*,

iii. Au vyote *Kifungo na Faini* tajwa hapo juu.


*(B). Adhabu kwa Wasafirishaji kwenda nje ya nchi.*

Kifungu/Kanuni Na. 8 (b) cha Sheria tajwa hapo juu kinataja Adhabu kwa Mtu au Watu hao kama ifuatavyo;

i. Faini isiyopungua *Milioni 5 na isiyozidi Milioni 20*,

ii. Kifungo Kisichozidi *Miaka 2*,

iii. Au vyote *Kifungo na Faini* tajwa hapo juu.


*(C). Adhabu kwa Wanaohifadhi na Wasambazaji*

Kifungu/Kanuni Na. 8 (c) cha Sheria tajwa hapo juu kinataja Adhabu kwa Mtu au Watu hao kama ifuatavyo;

i. Faini isiyopungua *Milioni 5 na isiyozidi Milioni 50*,

ii. Kifungo Kisichozidi Miaka 2,

iii. Au vyote *Kifungo na Faini* tajwa hapo juu.


*(D). Adhabu kwa Wauuzaji*

Kifungu/Kanuni Na. 8 (d) cha Sheria tajwa hapo juu kinataja Adhabu kwa Mtu au Watu hao kama ifuatavyo;

i. Faini isiyopungua *Laki 1 na isiyozidi Laki 5*,

ii. Kifungo Kisichozidi *Miezi 3*,

iii. Au vyote *Kifungo na Faini* tajwa hapo juu.


*(E). Adhabu kwa Watumiaji na Wanaomiliki*

Kifungu/Kanuni Na. 8 (e) cha Sheria tajwa hapo kinataja Adhabu kwa Mtu au Watu hao kama ifuatavyo;

i. Faini isiyopungua *Elfu 30 na isiyozidi Laki 2*,

ii. Kifungo Kisichozidi *Siku 7*,

iii. Au vyote *Kifungo na Faini* tajwa hapo.


NB:

SAMBAZA UJUMBE HUU KWENYE MAKUNDI MENGI NA KWA WATU WAKO WOTE ILI KUEPUKANA NA ADHABU ZISIZO ZA LAZIMA.

TUSAIDIANE KUTUNZA MAZINGIRA YETU.


Imeandaliwa na *Machibya Kapiga-Wakili*,

 *Wa kujitegemea ADVOCATES*

0744778869, kapiga2012@gmail.com


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa