• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SHIRIKA LA PADI LAPINGA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WATOTO

Tarehe ya kuwekwa: September 8th, 2020

Mkurugenzi Mtendaji “PADI” Iskaka Msigwa amesema Ukatili wa kijinsia ni kitendo anachofanyiwa mtu na mtu mwingine ambacho kinaweza kumsababishia madhara kimwili, kingono, kisaikolojia, na kiuchumi.

Msigwa ametoa kauli hiyo akiwa  katika mafunzo ya wakuu wa idara mbalimbali kutoka Manispaa yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea leo 08.09.2020.

 Awali alianza na kusema Tanzania Mission to the Poor and Disabled (PADI) ni Shirika la kiraia lenye lengo la kuwasaidia watu maskini, Wazee, na Walemavu lenye makao makuu Mjini Songea  ambalo limekuwa chachu ya maendeleo kwa Wazee kwenye Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma Nchini Tanzania.

Alisema PADI imeanza kutekeleza mradi mpya unaotambulika kwa jina la USAID Kizazi Kipya ambao unalenga kuibua vipaji vya watoto wenye umri wa miaka 9-14,  pamoja na  kuhamasisha watoto kupata  Elimu ya kuondoa unyanyasaji wa kijinsia. Aidha, ili kuwapata watoto hao shirika  litashirikisha taasisi za dini  ( Misikiti na Makanisa ), na  Shule kwa ajili ya  kuwapatia  Elimu ya Ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.

Aliongeza kuwa CBIM- Coaching Boys Into Men ni shughuli ambayo inatekelezwa mradi  ajili ya kuwafanya Wavulana wawe Wanaume Bora , Aidha  katika kutekeleza  utendaji wa kazi wa Mradi huu ambao walengwa ni watoto wataweza kushiriki  katika mchezo wa mpira wa miguu ambao watakuwa wanafundishwa na kocha ambaye atateuliwa na taasisi husika yaani shule,/ taasis ya dini ambaye pia atakuwa amepata mafunzo namna ya kusimamia michezo.

 Alibainisha kuwa michezo hiyo itafundishwa  kwa awamu 12,  na kwa kila siku baada ya  mafunzo hayo watatenga dakika 15 za  kufundisha nini maana ya Ukatili  ili waweze kufahamu madhara ya ukatili wa kijinsia, na baada ya mafunzo hayo zitatolewa zawadi kama begi la shule, daftari, peni, Viatu, na  Jezi za michezo kama motisha ya ushiriki wa mafunzo.

Naye Afisa ustawi wa Jamii Manispaa ya Songea Vicent Ndumbaro alisema  kuwa madhara ya ukatili wa kijinsia huathili uchumi, kimwili, kingono, na kisaikolojia ambapo alibainisha kuwa ili kutokomeza ukatili wa kijinsia nikuendelea kutoa Elimu kuhusu ukatili kijinsia kwa wazazi,  walezi, walimu, watoto, na jamii kwaujumla.

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa