• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SIKU 365 ZA RAIS SAMIA ZILIVYOBADILI SEKTA YA MALIASILI NA UTALII TANZANIA.

Tarehe ya kuwekwa: March 21st, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

21 MACHI 2022

Waziri wa Maliasili na Utalii  Dkt. Damas Ndumbaro (MB) amempongeza Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mapinduzi ya maendeleo ndani ya sekta ya Maliasili na Utalii nchini Tanzania.

Amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Ruvuma hapo jana Machi 20, 2022 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kwa lengo la kueleza mambo 10 muhimu yaliyofanywa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha siku 365 tangu aingie madarakani.

Alisema kuwa Serikali ya awamu ya sita imeongeza juhudi katika kuimarisha uhifadhi rasilimali  za wanyama pori ambapo kwa kipindi cha mwaka mmoja ujangili umepungua kwa asilimia 90% na kupelekea ongezeko kubwa la idadi ya Faru katika hifadhi mbalimbali nchini.

“Sekta ya Maliasili na Utalii imechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la  mapato na uchumi wa Taifa ambapo kwa kipindi cha siku 365 idadi ya watalii wa ndani imeongezeka kutoka kwenye watalii 562,549 hadi kufikia watalii 788,933 sawa na ongezeko la asilimia 40.2% na kuongeza mapato kutoka kwenye Bilioni 9.7 hadi Bilioni 12.4 kwa watalii wa ndani tu” Dkt. Ndumbaro alibainisha.

Aliongeza kuwa licha ya dunia kukumbwa na janga la UVIKO 19 hali iliyopelekea kushuka kwa shughuli za utalii kwa mataifa mengi, kwa nchi ya Tanzania idadi ya watalii kutoka nje imeongezeka kwa asilimia 48.6% na hivyo kuongeza mapato kutoka kwenye dola za kimarekani Milioni 714. 59 hadi kufikia dola za kimarekani Bilioni 1 sawa na asilimia 76%.

Serikali ya Awamu ya sita imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 90.2 kwa ajili ya kuimarisha miundombinu katika maeneo ya hifadhi za Utalii pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali kwa wadau pamoja na waongoza utalii nchini ambapo watu 150 kutoka kila Mkoa walipata fursa ya kushiriki mafunzo hayo.’Alieleza’

Dkt. Ndumbaro alisema kuwa “Rais Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo kwa kila Mkoa kuhakikisha wanaandaa matamasha ya utamaduni kwa lengo la kutoa chachu na kutangaza utalii ambapo kwa Mkoa wa Ruvuma Tamasha la Majimaji Serebuka litaanza kufanyika kimkoa pamoja na kuanzisha kumbukizi ya miaka 100 ya Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ili kuchochea uzalendo na kuibua miradi mbalimbali hasa katika maeneo ya hifadhi za Utalii”.

Pia, Serikali imefanikiwa kutafuta masoko ya Utalii nje na ndani ya nchi kwa kipindi cha siku 365 na kufanikiwa kuuza zaidi ya vitalu 79 vya uwindaji kwa mfumo wa kielektroniki pamoja na kuwekeza juhudi kubwa ya kuendeleza sekta ya misitu na  Nyuki kwa kuunda sheria ndogo inayoruhusu usafirishaji wa mkaa mbadala nje ya nchi pamoja na kuanzisha ujenzi wa viwanda vya kuchakata mazao ya Nyuki ambapo miongoni mwa wanufaika wa viwanda hivyo ni Manispaa ya Songea.

Alieleza kuwa Nchi ya Tanzania imefanikiwa kutambulika na kupewa heshima katika nyanja ya Utalii duniani kwa kupokea Tuzo zaidi ya kumi kutoka katika mashirika makubwa duniani ikiwemo na Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Utalii (UNWTO) ambapo hata hivyo bado Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imejipanga kuendelea kuitangaza Tanzania nje na ndani ya nchi kwa kuingia mikataba na mashirika mbalimbali ya kimataifa ikiwemo na shirika la ndege la Emirates. “Alibainisha”

Ametoa rai kwa waandishi wa habari kuendelea kuhamasisha jamii katika kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi linalotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.

Kwa upande wao waandishi wa habari wametoa pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Mh. Waziri kwa kusimamia vizuri utekelezaji  katika sekta ya Maliasili na Utalii na kuiomba Serikali kuboresha vivutio vya Utalii vilivyopo Mkoani Ruvuma.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa