• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SIKU YA WAZEE DUNIANI

Tarehe ya kuwekwa: October 1st, 2024

Wataalamu wa ustawi wa jamii wametakiwa kuendeleza utaratibu wa kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kuwajali,kuwatunza, na kuwapenda wazee, pamoja na jamii kutambua haki wanazostahili wazee na wajibu wa wazee katika jamii, kwasababu kuna baadhi ya maeneo bado wazee wakikumbwa na changamoto ya kufanyiwa ukatili ikiwemo kupigwa,kunyimwa chakula,kutukanwa kudhalauliwa na kutuhumiwa washirikiana hali inayowapelekea waishi maishaya hofu.

Hayo yameelezwa na katibu tawala  wilaya ya Songea Mtella Mwampamba wakati akihutubia katika adhimisho la siku ya wazee duniuani lililofanyika katika viwanja vya majimaji manispaa ya Songea nakuhudhiliwa na Viongozi wa mabaraza ya wazee manispaa ya Songea,mstahiki meya,Mkurugenzi wa manispaa,Wakuu wa idara, Wakuu wa madhehebu ya dini na Viongozi wa vyama vya siasa, ambapo  amewataka wananchi kutambua umuhimu wa wazee katika jamii zao.

Tarehe 1 october Kila mwaka ni siku ya wazee Duniani na siku hii ilianzishwa kwa lengo maalumu la kuhakikisha jamii inajengewa uelewa na hamasa kuhusu kulinda haki ustawi,na maslahi ya wazee, kila mwaka Tanzania huungana na nchi nyingine za umoja wa mataifa katika kuadhimisha siku hii muhimu kwa ustawi wa  wazee.

Maadhimisho ya siku ya wazee duniani mwaka 2024 yamebeba kauli mbiu isemayo TUIMARISHE HUDUMA KWA WA ZEE: WEKEZA KWA HESHIMA. Kauli mbiu hii imelenga kuelimisha jamii juu ya  umuhimu wa kuwasaidia wazee katika kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo katika maisha ya kila siku.

Wazee wanastahili kupata haki zao za msingi katika jamii kama binadamu wengine bila kubaguliwa, haki hizo ni haki ya kuwa huru, haki ya kushiriki na kushirikishwa, haki ya kutuzwa , haki ya kujiendeleza, haku ya kuheshimiwa, haki ya kusikilizwa, haki ya kulindwa, haki ya kujumuika na makundi mengine, haki ya kuabudu dini waipendayo ilimradi hawavunji sheria, haki ya kupendwa, haki ya kugombea nafasi ya uongozi,haki ya elimu, haki yakupata huduma za afya, haki ya kupata chakula pamoja na mavazi na chakula.

Manispaa ya Songea inatekeleza sera ya afya ya mwaka 2007 na sera ya Taifa ya wazee ya septemba 2003 kwakutoa huduma za matibabu bila malipo kwa wazee. Halimashauri ya manispaa ya Songea  kwa kipindi cha mwaka wa fedha kuanzia tarehe 01/07/2023 hadi 30/06/2024  imefanikiwa kutoa huduma za matibabu bure kwa wazee wapatao 7204.[Me 3239 na Ke 3965]. Gharama ya fedha zilizotumika katika matibabu ya wazee ni shilingi 34,950,000/=.

 IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.                                                                                                                                            






Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Tazama zote

Video

Makabidhiano ya Mkataba Soko la Manzese A&B
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa