• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Kupambana na Matapeli.

Tarehe ya kuwekwa: July 29th, 2021

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma wameawataka Wananchi  kutoa taarifa  inayoweza kusaidia kukamatwa kwa matapeli ambao wamekuwa wakiwarubuni wananchi kwa kutumia majina ya Maafisa wa TAKUKURU kwa kuwapigia simu na kuwatishia kuwa wanatuhumiwa na wamekuwa wakiwaomba fedha, Kwa yeyote anayetambua amekuwa akifanya jambo hilo Mkoani Ruvuma anatakiwa  kuacha mara moja.”

Hayo yamebainishwa  na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Hamza Mwenda  akiwa katika  kikao na Waandishi wa Habari kilichofanyika leo 29.07.2021 ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma  ambacho  ilisomwa taarifa utekelezaji  wa ufuatiliaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika  kipindi cha miezi mitatu Aprili hadi Juni 2021.

Mwenda alisema Lengo kuu  la ufuatiliaji  huo ni kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kiwango bora kinachotakiwa,  kinachoendana na thamani ya fedha pia na kuzuia mianya ya rushwa pamoja na upotevu wa rasilimali katika utekelezaji wake.

Alisema katika kipindi cha miezi mitatu wameweza kufanya kazi ya uimarishaji wa mifumo kwa kufanya chambuzi nne 4 za  mifumo, pamoja na kufanyika kwa Warsha 5  tano za wadau zilizofanyika kwa ajili ya kutekeleza  maazimio ya wadau yaliyoazimiwa kupitia  vikao vya warsha, na kufanikiwa kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo (PETS) tano  5  yenye thamani ya shilingi 1,002,749,177/=.

Aidha, katika kipindi cha miezi mitatu TAKUKURU Mkao wa Ruvuma ilipokea kesi 110 ambazo kesi 39 zilihusu  Rushwa, kesi 71  hazikuhusu rushwa hivyo watoa taarifa walishauriwa namna bora ya kuzitatua kero zao kupitia mamlaka husika.

Akitaja idara zilizolalamikiwa katika kipindi cha miezi mitatu ni pamoja na  Viongozi wa Serikali za Mitaa/Vijiji 22, Idara ya fedha kupitia Halmashauri za Wilaya   20,  Elimu 12, Polisi  9, Ardhi 9, Taasis za Fedha 8, Kilimo 6, Mahakama 5, sekta binafsi 4, vyama vya ushirika 3, ulinzi  3, Afya 3, Hifadhi ya jamii 4, na maji 2 ambapo katika kipindi hicho majalada ya uchunguzi 39 yalifunguliwa na kati ya hizo, majalada 17 wameweza kukamilisha. “Mwenda alibainisha”.

Alisema katika kutekeleza majukumu yake katika robo ya nne ya mwaka  2020/2021 TAKUKURU imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kwa kutumia njia  ya Semina kuelimisha umma katika ofisi za umma na binafsi na hata mashuleni,  Mikutano ya hadhara kwa kutumia TAKUKURU INAYOTEMBEA, kuonyesha  maonyesho  hususani siku ya wanawake duniani, mbio za mwenge,  magulio pamoja  na mashuleni, na  kuimarisha klabu za wapiga Rushwa.

 MWISHO, Amewataka wananchi wote Mkoani Ruvuma kuchukua hatua mahususi  wanapoona kuna dalili au ukiukwaji wa sheria zetu za nchi au viashiria vya vitendo vya rushwa na kutoa taarifa TAKUKURU.

 

Na; 

AMINA PILLY;

AFISA HABARI – SONGEA MANISPAA.

29 julai 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa